KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

December 29, 2014

CCM,CHADEMA WAISHAMBULIA SERIKALI

 

 Dar es Salaam. Katibu mkuu wa Chadema, Dk Willbrod Slaa(pichani) amedai kuwa nchi inayumba kwa sababu Serikali inakumbatia wawekezaji wezi na wasiojali maslahi ya Watanzania.
Amesema hilo lilidhihirika wakati Rais Jakaya Kikwete alipokuwa akilihutubia Taifa kupitia Wazee wa Mkoa wa Dar es Salaam, kwa kuwatetea wawekezaji huku akijua baadhi yao siyo waaminifu.
Akizungumza na wakazi wa Kata ya Tegeta katika mkutano wa hadhara uliolenga kutatua kero za wakazi wa Tegeta Magereji, Dk Slaa alisema: “Hata wakazi wa Magereji mnataka kuhamishwa kutoka eneo lenu la biashara na mwekezaji ambaye tulimtaja katika orodha ya mafisadi wa nchi hii mara nyingi tu. Rais Kikwete anatakiwa kutambua kuwa Watanzania wamewachoka wawekezaji wezi, tunataka wawekezaji watakaowanufaisha wananchi.”
Alisema zaidi ya Sh1 trilioni za Meremeta, Richmond na Escrow zimeibwa na wawekezaji. “Nchi haiwezi kutafunwa kila siku halafu sisi tunakaa kimya. Haki inaweza kucheleweshwa tu, lakini itapatikana.”
Kuhusu mgogoro wa eneo hilo la Tegeta Magereji, Dk Slaa alisema Chadema wataweka mawakili wao atakayeshirikiana na wa upande wa walalamikaji, kwa lengo la kuhakikisha wananchi hao wanapata haki yao.
Mgogoro wa Mtaa wa Magereji ulianza takribani miaka mitano iliyopita baada ya mafundi magari waliohamishwa na Manispaa ya Kinondoni kupelekwa eneo hilo na baadaye kutakiwa kuhama kwa madai kuwa eneo hilo limechukuliwa na wawekezaji.
Katika mkutano huo alikuwapo pia mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Madale kwa tiketi ya CCM, Gratian Mbelwa ambaye aliungana na Chadema kukemea dhuruma wanayotaka kufanyiwa wananchi hao na Serikali huku akidai kuwa inachochewa na baadhi ya watendaji wa Serikali Kuu.
Mbelwa alisema wakazi hao wamewekeza zaidi ya Sh35 bilioni katika eneo hilo, lakini wanatakiwa kulipwa fidia ya mifuko 10 ya saruji kila mmoja jambo lililoelezwa kuwa ni sawa dhuluma. Eneo hilo lina watu 4,000.
Huku akiwa amevalia sare za CCM, Mbelwa alisema mgogoro wa Tegeta Magereji ni sawa na Tegeta Escrow nyingine, kauli iliyowafanya wananchi wamshangilie.
Mbelwa alisema mpaka sasa wananchi wamechangishana zaidi ya Sh70 milioni kwa ajili ya kuendesha kesi hiyo.
Katika mkutano huo, Dk Slaa alijibu maswali matano kutoka kwa wananchi huku akimtupia lawama Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Jordan Rugimbana na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaamm Saidi Meck Sadiki kwa kuulea mgogoro huo.
Alisema hata Rais Kikwete anaujua mgogoro huo kwa muda mrefu, lakini ameamua kukaa kimya bila kuuzungumzia kila anapozungumzia migogoro iliyoko nchini.CREDIT MWANANCHI

No comments:

Post a Comment