Rais
wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein
(katikati) akiongoza matembezi ya Siku ya Kilele cha Mazoezi ya Viungo
Kitaifa akiwa na Viongozi wengine yaliyoanzia katika Uwanja wa Tumbaku
hadi Uwanja wa Amaan Studium leo asubuhi ambapo yamejumuisha Vikundi
mbali mbali vya Unguja na Pemba.
Miongoni
mwa vikundi vilivyoshiriki katika matembezi ya Siku ya Kilele cha
Mazoezi ya Viungo Kitaifa ni kikundi cha KVZ Fitness Group kikiwa katika
hali ya ukakamavu na nidhamu ya juu wakipita katika barabara Kariakoo
kuelekea Komba wapya ambapo Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la
Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein aliyaongoza matembezi hayo leo asubuhi.
Kundi
la Mazoezi Zoni C wakiwa na bango lao linalosomeka "Siku ya Mazoezi
Kitaifa 01Jan 2015 Mazoezi ni Tiba Mbadala",kama wanavyoonekanwa wakiwa
katika matembezi ya Siku ya Kilele cha Mazoezi ya Viungo Kitaifa leo
yaliyoongozwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi
Dk.Ali Mohamed Shein (hayupo pichani)
No comments:
Post a Comment