KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

January 21, 2015

KAMANDA WA KONY AFIKISHWA THE HEAGUE

Ongwen kulia akiwa na kamanda mkuu wa kikosi cha Afrika kinachomsaka mkuu wa kundi la LRA Joseph Kony
Kamanda mkuu wa kundi la waasi la LRA nchini Uganda Dominic Ongwen amewasili mjini Hague ambako atafunguliwa mashitaka ya uhalifu wa kivita.
Ongwen, alikuwa kamanda mwenye kuogopewa sana katika kundi la waasi la LRA na alikamatwa katika Jamhuri ya Afrika ya Kati mapema mwezi huu.
Uganda ilikubali kwamba muasi huyo apelekwe katika mahakama ya kimataifa ya ICC, licha ya nchi hio kuwa mkosoaji mkubwa wa mahakama hio.
Wanajeshi wa Marekani wakishirikiana na wa Afrika, wamekuwa wakifanya msako dhidi ya Ongwen tangu mwaka 2011.
Anasemekana kua naibu wa kiongozi wa LRA Joseph Kony ambaye bado yupo mbioni.
ICC ilisema kwamba Ongwen atazuiliwa katika kituo kimoja nchini Uholanzi hadi mahakama itakapokuwa tayari kusikiliza kesi yake.
Alitarajiwa kufanyiwa uchunguzi wa kimatibabu alipowasili Hague huku tarehe ya kusikilizwa kwa kesi yake ikisubiriwa.
Taarifa ilitolewa na Baraza la usalama la Umoja wa Mataifa pamoja na katibu mkuu wa umoja huo ikipongeza hatua ya kumpeleka Ongwen mjini Hague.
Ban alisema ni hatua kubwa katika kuhakikisha kwamba waaathiriwa wa unyama uliotendwa na LRA wanapata haki.

No comments:

Post a Comment