Mkaguzi
na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali Prof. Mussa Juma Assad akisoma
hotuba ya kumkaribisha mgeni rasmi wakati wa Mkutano wa Pili wa Baraza
la Wafanyakazi wa Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi uliofanyika jana katika
Ukumbi wa Hoteli ya Naf Beach iliyoko mkoani Mtwara.
Mgeni
rasmi, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Utawala Bora Mhe. George Mkuchika,
akiwahutubia wajumbe wa Baraza la Pili la Wafanyakazi wa Ofisi ya Taifa
ya Ukaguzi muda mchache kabla ya kulifungua baraza hilo jana katika
Ukumbi wa Hoteli ya Naf Beach iliyoko mkoani Mtwara.
Wajumbe
wa Baraza la Pili la Wafanyakazi wa Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi
wakimsikiliza kwa makini Mgeni rasmi, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais,
Utawala Bora Mhe. George Mkuchika (hayupo pichani) wakati wa mkutano wa
baraza hilo uliofanyika jana katika Ukumbi wa Hoteli ya Naf Beach
iliyoko mkoani Mtwara. (PICHA ZOTE NA SARAH REUBEN - OFISI YA TAIFA YA
UKAGUZI).





No comments:
Post a Comment