KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

January 31, 2015

MTALAAM WA SILAHA ZA KEMIKALI WA IS AUAWA

Mlipuko
 Jeshi la Marekani linasema kuwa mtaalamu mmoja wa silaha za kemilkali aliyekuwa akifanya kazi na kundi la Islamic State ameuawa kwenye mashambulizi ya muungano nchini Iraq.
Marekani inasema kuwa kifo cha mwanamume huyo kwa jina Abu Malik kitavuruga uwezo wa kundi hilo wa kuunda na kutumia silaha za kemikali.
Abu Malik anaripotiwa kufanya kazi kama mtaalamu wa silaha za kemikali kwa rais wa zamani wa Iraq Sadam Hussein kabla ya uvamizi ulioongozwa na Marekani mwaka 2003.
Kundi la Islamic State hudhibiti maeneo makubwa nchini Syria ambapo serikali imekuwa ikiharibu silaha za kemikali.

No comments:

Post a Comment