KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

January 20, 2015

VURUGU ZAIBUKA KUMPINGA KABILA

Rais Kabila amekuwa mamlakani tangu mwaka 2001

Polisi katika Jamuhuri ya kidemokrasi ya Congo, wamefyatua risasi hewani ili kuwatawanya waandamanaji waliokuwa wamekusanyika katika mji mkuu Kinshasa kupinga sheria mpya ya uchaguzi.
Serikali inasema kuwa watu wanne walifariki katika vurugu za Jumatatu ingawa upinzani unasema idadi huo huenda ikwa kujuu kuliko iliyonakiliwa.
Wanafunzi wameweka vizuizi barabarani na pia wameshuhjudiwa wakichoma magurudumu, katika barabara zinazoelekea katika chuo kikuu mjini humo.
Wanatuhumu wanasia wanaomuunga mkono Rais Joseph Kabila ambaye muhulka wake wa pili unatarajiwa kumalizika mwaka ujao kwa kujaribu kujiongeza muda mamlakani kwa kuidhinisha mipango ya kufanyika sensa ambayo itachelewesha uchaguzi kwa miaka mingi.
Vurugu hizi zinashuhudiwa huku baraza la Senate likidadisi mswada ambao huenda ukasababisha Rais Kabila kuongezwa muda mamlakani.

No comments:

Post a Comment