KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

January 21, 2015

WARIOBA:KURA YA MAONI APRILI NI NDOTO

Aliyekuwa Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba, ametabiri kukwama kwa kura ya maoni kuhusu Katiba pendekezwa, akieleza kuwa maandalizi hafifu ambayo yamefanyika hadi sasa hayaruhusu zoezi hilo kufanyika.
Aidha, amesema iwapo kutatokea ujanja ujanja wowote wa kutaka kukiuka sheria ya kura ya maoni, nchi itaingia kwenye matatizo.

Akizungumza katika mahojiano na NIPASHE jana, Jaji Warioba alisema wiki iliyopita, wajumbe wa iliyokuwa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, walikutana na majadiliano yao yalijikita kwenye maandalizi ya kura ya maoni kuhusu Katiba pendekezwa.

Alisema sheria namba tatu ya mwaka 2014, ambayo inahusu kura ya maoni inaeleza kuwa jambo la kwanza kufanyika ni uboreshaji wa daftari la wapigakura, ambalo utafuatiwa na elimu kwa umma kwa miezi miwili kisha kampeni kwa mwezi mmoja.

“Tukaona kuna umuhimu wa kufanya maandalizi kwa umakini mkubwa kabisa, tumeichambua sheria hii ya kura ya maoni, tumeona mahitaji ya sheria hii lakini utaratibu wa sheria hauanzi mpaka Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), imeanza aundikishaji wa wapigakura,” alisema.

ELIMU KWA UMMA
Akizungumzia msingi wa elimu kwa umma, Jaji Warioba alisema NEC inapaswa kufanyakazi hiyo kwa kushirikiana na asasi za kiraia kwa kipindi kisichopungua miezi miwili ili kuwaelimisha wananchi nini kilichopo ndani ya Katiba na utaratibu wa kura ya maoni.

“Kwa hiyo tuna miezi mitatu, ratiba iliyowekwa na serikali inasema wanakamilisha kuandikisha Machi kisha kampeni inaanza mara moja. Kipindi cha elimu hakikuwekwa kwenye ratiba. Mimi nafikiri ni vizuri kufuata sheria kwa sababu tukiendesha hii kinyume cha sheria inaweza kuleta matatizo,” alisema.

Jaji Warioba aliongeza kuwa: “Na kama tukifuata sheria inavyosema, ni kwamba NEC ikimaliza kazi Machi; Aprili na Mei itakuwa ni elimu, Juni ni kampeni kwa hiyo kura ya maoni itakuwa ni Julai.”

 Hata hivyo, alisema kura hiyo kufanyika Julai ni matatizo kwa sababu ni wakati ambao maandalizi ya uchaguzi mkuu yatakuwa yameanza na itakuwa kipindi vyama vya siasa vinakuwa vinateua wagombea wake.

“Ukafanye yote kwa pamoja inaweza kuleta matatizo lakini muhimu tunalosema tuifuate sheria kuwepo na kipindi cha elimu kwa umma.”

No comments:

Post a Comment