KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

February 1, 2015

LIPUMBA AHUTUBIA BILA POLISI

 

Mwenyekiti wa CUF, Prof Ibrahim Lipumba, akizungumza kwenye mkutano wa hadhara, uliofanyika katika Viwanja vya Manzese Argentina, Dar es Salaam jana. Picha na Emmanuel Herman

Siku tano baada ya kuzuiwa kufanya mkutano wa hadhara kwa madai ya tishio la ugaidi, Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba jana alihutubia wananchi eneo la Manzese jijini Dar es Salaam bila kuwapo kwa ulinzi wa Jeshi la Polisi.
Mkutano wa jana wa Profesa Lipumba, ambaye alijikuta kwenye matatizo na Jeshi la Polisi baada ya kupigwa, kutiwa mbaroni na baadaye kufunguliwa mashtaka Jumanne iliyopita, jana ulitawaliwa na amani na ulidumu kwa takriban saa mbili kwenye eneo hilo la Manzese ambalo kwa kawaida huwa na utitiri wa watu.
Profesa Lipumba alikutwa na kadhia hiyo wakati akielekea Zakhem, Mbagala ambako alidai kuwa alikuwa akienda kushawishi wananchi watawanyike kwa amani baada ya Jeshi la Polisi kuzuia maandamano na mkutano wa hadhara.
Katika tukio hilo, mwenyekiti huyo wa CUF alikamatwa pamoja na wafuasi 32 na baadaye kufunguliwa mashtaka ya kula njama, kufanya maandamano na kukusanyika bila ya kibali. Vitendo hivyo vya polisi vilisababisha Bunge la Jamhuri ya Muungano kusitisha shughuli zake na kuamua kujadili tukio hilo, bila ya kujali kuwa lilikuwa likiingilia shughuli za mhimili mwingine wa nchi.(P.T)

Katika mkutano wa jana, hakukuwa na polisi waliovalia sare kama ilivyo kawaida kwenye mikutano ya hadhara ya kisiasa, hasa ya vyama vikubwa vya upinzani, ambayo hulindwa na askari wenye silaha na jana jukumu hilo lilifanywa na kikosi cha ulinzi cha chama hicho cha Blue Guards.
Alipotafutwa Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Kinondoni, Camillius Wambura alisema hafahamu kuhusu suala hilo kwa kuwa yuko nje ya eneo lake la kazi.
"Hilo silijui kwani nipo nje ya Dar es Salaam hivyo siwezi kulizungumzia," alisema Kamanda Wambura, ambaye alieleza kuwa yuko Dodoma ambako kulikuwa na mkutano wa maofisa waandamizi wa Jeshi la Polisi uliomalizika jana.SOMA ZAIDI CHANZO MWANANCHI

No comments:

Post a Comment