KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

February 21, 2015

MFUKO WA UMOJA-FURSA KWA WATANZANIA KUPATA FAIDA

Na Mwandishi Wetu
Mfuko wa Umoja umeweza kuwanufaisha Watanzania wengi na taasisi zilizowekeza kwa kutoa faida kubwa tokea kuanzishwa kwake, Mfuko huu unaendeshwa na Dhamana ya Uwekezaji Tanzania ((UTT-AMIS) ambayo ni taasisi iliyo chini ya Wizara ya Fedha iliyoanzishwa 2003.
Moja ya majukumu ya Dhamana ni kuwawezesha Watanzania kushiriki katika masoko ya fedha, kuhamasisha uwekaji wa akiba na kuendesha mifuko  ya uwekezaji wa pamoja kwa gharama nafuu .
Mkurugenzi wa Masoko wa  UTT-AMIS,Daud Mbaga, anasema kuwa  Watanzania wanawezeshwa kwa kuweka akiba kulingana na uwezo wao huku wakipata faida kutokana na uwekezaji kwenye masoko ya mitaji na dhamana.
“Ili kuweza kushiriki katika uwekezaji kupitia Dhamana mwekezaji anatakiwa kununua vipande ikiwa ni sehemu ya umiliki wa mwekezaji kwenye mfuko husika,” anasema.
 Anafafanua kuwa toka kuanzishwa kwake hadi sasa Dhamana imeweza kuanzisha mifuko mitano (5) ambayo ni Umoja, Wekeza Maisha, Jikimu, Watoto na Ukwasi.
“Watanzania wameweza kujiunga kwenye mifuko inayoendeshwa na Dhamana ili kupata faida zitokanazo na uwekezaji kwenye masoko ya mitaji na dhamana,”anafafanua.
Anasema Mfuko wa Umoja ndio mfuko wa kwanza kuanzishwa na ulianza kuuza vipande mwezi Mei, 2005. Ni mfuko wenye amana kubwa ambao kwenye mauzo ya mwanzo uliweza kukusanya zaidi ya Shilingi bilioni 90 na kuvunja rekodi ya mauzo ya mwanzo (IPO) Afrika Mashariki nzima.

No comments:

Post a Comment