KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

February 19, 2015

UTEUZI WA DC MAKONDA WAZUA GUMZO

MAKONDA1
Na Andrew Chale wa modewji blog
Ikiwa ni siku moja tu tangu kutangazwa kwa wakuu wapya wa Wilaya mbalimbali za Tanzania Bara, Uteuzi uliofanywa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Jakaya Mrisho Kikwete ikiwemo kumteua kada wa Chama cha Mapinduzi anayetokea Jumuiya ya Vijana (UVCCM), Paul Makonda kuwa Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni,  watanzania wengi wamebeza uteuzi huo huku wengine wakiunga  mkono.
Modewji blog  iliweza kuongea na watu mbalimbali juu ya maoni yao kufuatia uteuzi huo wa Rais kwa kumchagua Makonda. 
Wakizungumza kwa nyakati tofauti jijini Dar es Salaam baadhi ya wasomaji wa mtandao huu, Sued Musa mkazi wa Kawe alibainisha kuwa, uteuzi huo wa Rais ni mzuri ila  alikosea kumweka wilaya ya kama Kinondoni yenye matatizo chungu mzima ya kiutendaji ikiwemo migogoro ya mipaka, ardhi, wafanyabiashara ndogondogo na mambo mengine ya ndani.
“Tunampongeza Rais kwa kuteua wakuu wapya wa mikoa, ila kwa huyu Paul Makonda kumweka Kinondoni, ameteleza. Hii wilaya inahitaji mtu mwenye uzoefu mkubwa katika uongozi na uadilifu” alisema Sued Musa.
Kwa upande wake, Jamal Tamba mkazi wa Kigogo, jijini Dar es Salaam,  alisema kuwa uteuzi huo ni mpya hivyo tuwape muda wateule wote wa Rais na tutaona utendaji wao kama wanafaa ama lah!, alieleza.
Hata hivyo, kwa upande wa mitandao ya kijamii baadhi ya watu wameweza kutoa maoni yao mbalimbali ambayo hata hivyo wengi wao wameyatoa kwa kile wanachokijua wao ikiwemo masuala ya maslai ya kisiasa.


No comments:

Post a Comment