Mwamuzi wa kimataifa wa Tanzania
mwenye beji ya FIFA, Israel Mjuni Nkongo amechaguliwa kuchezesha mchezo
wa Ligi ya Mabingwa Afrika (CL) kati ya wenyeji Zesco FC ya Zambia dhidi
ya AS Kaloum ya Guinea.
Katika mchezo huo wa kwanza wa mzunguko
wa pili, Nkongo atasaidiwa na washika kibendera John Kanyenye na
Josephat Bulali na mwamuzi wa akiba Waziri Sheha wote kutoka Tanzania,
huku Kamisaa wa mchezo akiwa Mayixole Elvin Shishana kutoka nchini
Afrika KusiniMchezo huo unatarajiwa kufanyika kati ya tarehe 13,14,15 Machi mwaka huu nchini Zambia.
No comments:
Post a Comment