Na Jonas Mushi, Dar es Salaam
MAMLAKA ya Hali ya Hewa nchini (TMA), imesema mvua ya mawe iliyonyesha Jumanne wiki hii wilayani Kahama na kusababisha vifo vya watu 46 na wengine 80 kujeruhiwa haikuwa ya kawaida katika ukanda huu wa kitropiki.
Mamlaka hiyo imetanabahisha kuwa iliona hali ya kuwepo kwa tonado (barafu) katika eneo la ukanda wa Ziwa Victoria nusu saa kabla ya mvua hiyo kunyesha.
Akitoa taarifa kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu, Mkurugenzi Mkuu wa TMA, Dk. Agnes Kijazi, alisema kabla ya mvua hiyo Mamlaka ilitoa utabiri wa saa 24 ulioonyesha kuwepo kwa wingu zito pamoja na radi katika eneo la ukanda wa Ziwa Victoria.
Alisema nusu saa kabla ya kutokea kwa tonado, mitambo ya TMA iliona hali hiyo iliyosababishwa na kushuka kwa barafu katika usawa wa dunia na kushindwa kuyeyuka, hivyo kutokana na upepo na ngurumo za radi iliyokuwepo, barafu hizo zikadondoka kabla hazijayeyuka.
No comments:
Post a Comment