KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

March 3, 2015

TMA:UKAME KUISHAMBULIA NCHI


NA WILLIAM SHECHAMBO
 KIWANGO cha mvua katika msimu wa mwaka huu wa masika ni kidogo kwenye maeneo mengi ya nchi hali inayoweza kusababisha ukame endapo Watanzania hawatazitumia kwa busara mvua chache zinazotarajiwa kunyesha nchini. Utabiri wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), juu ya mwelekeo wa mvua kwa kipindi cha miezi mitatu kuanzia sasa, ulisema licha ya maeneo mengi ya nchi kutarajia mvua za wastani, maeneo mengine mvua zitakuwa kubwa. Baadhi ya maeneo hayo ni kanda ya Ziwa Viktoria, mikoa ya Kagera, Simiyu na mikoa ya kusini mwa nchi ukiwemo Lindi, Ruvuma, Mtwara na Mashariki mwa mkoa wa Mbeya. Akizungumza na waandishi wa habari ofisi za TMA, Dar es Salaam jana, Mkurugenzi Mkuu wa wa Mamlaka hiyo, Dk. Agnes Kijazi, alisema kwa mwaka huu masika inakuja na mvua chache kutokana na mabadiliko ya tabia nchi. Dk. Agnes alisema pia licha ya mabadiliko hayo, ambayo wengi walitarajia unafuu wa hali ya hewa katika kipindi hiki ambacho maeneo mengi likiwemo jiji la Dar es Salaam joto limekuwa juu.UHURU

No comments:

Post a Comment