KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

April 6, 2015

FILIKUNJOMBE AIFAGILIA NEC

Mbunge  wa  jimbo la  Ludewa Deo Filikunjombe akishiriki ibada ya pasaka na  waumini wa kanisa  la RC Mavanga jimboni kwake.
 
MBUNGE wa   Ludewa  Deo Filikunjombe aipongeza  tume ya taifa  ya uchaguzi (NEC) Kwa kusogeza  mbele zoezi la upigaji kura  za maoni kwa katiba inayopendekezwa na  kuwa  hatua iliyofikiwa katika mchakato  huo ni kubwa na kumbukumbu kubwa kwa Rais Jakaya Kikwete anapoondoka madakarani na urithi kwa Rais ajaye kuendeleza mchakato  huo.

Filikunjombe  alitoa pongezi  hizo wakati akitoa salamu  zake za pasaka jana kwa waumini  wa madhehebu mbali mbali ya  Kikristo  katika  wilaya  ya  Ludewa   salam zilizoambatana na msaada  wa  viti  ,bati ,vinada  na saruji katika makanisa   hayo kama moja  ya utekelezaji  wa ahadi  zake kwa  madhehebu  hayo kama ambavyo  walivyomuomba .

Alisema  kuwa hatua  ya tume  ya taifa ya  uchaguzi  kuongeza  muda katika zoezi hilo la kura  za  maoni kwa  katiba inayopendekezwa mbali yakuwapunguzia majukumu  watanzania ya kufanya mambo  mengi kwa wakati mmoja bado kusogezwa  huko  mbele kutawafanya watanzania hasa wananchi  wake  wa ludewa kuendelea na shughuli  nyingine  za uzalishaji mali.

'hakuna uharaka  wa  kuharakisha  zoezi la  upigaji kura za maoni katika katiba  inayopendekezwa kwani hadi  sasa hatua iliyofikiwa ni  nzuri na kumbukumbu  kubwa kwa rais Jakaya kikwete anapomaliza  muda  wake kuwa amefanya jambo  hilo  kubwa hadi lilipoishia na Rais ajaye ataanzia alipoishia kikwete kwa kukamilisha katiba   hiyo  kuliko kukimbizana kama ilivyopangwa awali kabla ya tume kusogeza  mbele  zoezi hilo kwa  muda usiofahamika'
   . . 

No comments:

Post a Comment