KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

April 4, 2015

GARRISSA WAANDAMANA KUIPINGA AL- SHABAAB


Maandamano Garissa
 Wananchi wa mji wa Garissa nchini Kenya wamefanya maandamano kupinga vitendo vya kundi la Al Shabaab, lililoshambulia chuo kimoja kikuu mjini humo na kuwaua watu 147 wengi wao wakiwa wanafunzi hapo jana.
Waandamanaji pia wameelezea kutoridhika na vyombo vya usalama nchini humo wakisema havikuchukua hatua za kutosha kutoa ulinzi kwa waliouawa na kwa raia wengine kwa jumla.
Wazazi, jamaa na marafiki wa wanafunzi waliouawa katika chuo kikuu cha Garissa wamekuwa wakiendelea kuwasili katika eneo hilo kuitambua miili ya wapendwa wao.
Waliojeruhiwa wanaendelea kupata matibabu .

No comments:

Post a Comment