KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

April 27, 2015

GWAJIMA AJA KIVINGINE


Askofu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima  
Dar es Salaam, Askofu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima ameliombea Taifa ili liepukane na ajali za barabarani, akisema nyingi zinasababishwa na kafara zinazofanywa na baadhi ya watu aliowaita wabaya.
Akitoa mahubiri kwa mamia ya waumini wa kanisa hilo jana, Gwajima alisema ajali nyingi si za kawaida, bali ni makafara yanayotolewa na baadhi ya watu na kutaka kila mmoja kuliombea Taifa ili kuondokana na tatizo hilo.
Gwajima ambaye anatuhumiwa kwa kuachia silaha katika mikono isiyo salama pamoja na kumkashifu, Askofu Mkuu wa Kanisa Katoliki Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo, alisema takwimu za Kikosi cha Usalama Barabarani zinaonyesha kwamba tangu Januari hadi Machi, mwaka huu, watu 866 walikufa kwa ajali za barabarani na wengine 2,370 kujeruhiwa.
“Ni lazima tujiulize ni kwa nini watu wengi wamekufa kwa ajali mwaka huu, haya ni makafara yanayotolewa na watu, naomba makafara yawarudie wenyewe waliyoyatengeneza,” alisema bila kutaja majina.
Alisema idadi ya watu waliokufa ni ya kuishia Machi na kwamba idadi ya Aprili ikiongezwa, itaongezeka karibu mara mbili.
Katika takwimmu za Gazeti hili, kwa mwezi Aprili pekee, ajali zilizoripotiwa zimeua watu 104 hadi kufikia Aprili 17.
Gwajima alisema kuna sababu nyingi ambazo zimekuwa zikitolewa kuwa zinasababisha ajali za barabarani na kwamba Serikali inatakiwa kutafakari kwa kina.
“Wanasema ajali zinasababishwa na madereva walevi, kwani miaka iliyopita hakukuwa na walevi, wanasema madereva hawana mikataba ya ajira, mwaka jana walikuwa nayo hiyo mikataba, tujiulize kwa nini sasa?” alisema.

No comments:

Post a Comment