KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

April 27, 2015

UKAWA WAGAWANA MAENEO

Dar/Mikoani. Katika kile kinachoonekana kuendelea kujiimarisha kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Oktoba, vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) vimegawana maeneo mbalimbali nchini vikifanya mikutano ya hadhara na mafunzo kwa viongozi wake ikiwa ni utekelezaji wa mkakati wa ushindi.
Ukawa unaundwa na vyama vya Chadema, NLD, NCCR-Mageuzi na CUF.
Chadema kilianza ziara zake mikoani wiki zilizopita baada ya kuzindua mkakati wake uitwao ‘Hakuna kulala, Hakuna kula, Mpaka Kieleweke’ nchi nzima wakati timu ya NCCR-Mageuzi ikiweka kambi mkoani Kigoma kwa kile ilichokiita kuimarisha majimbo ya kimkakati.
Sanjari na vyama hivyo, CUF tangu juzi kiliingia katika moja ya ngome zake, mkoani Mtwara pamoja na mipango mengine ya kiushindi, kinahamasisha wananchi kujitokeza kujiandikisha kupiga kura.
Jitihada za Ukawa kuzunguka mikoani zinakuja ikiwa ni majuma kadhaa tangu Chama cha Mapinduzi (CCM) kikiongozwa na Katibu Mkuu wake Abdulrahman Kinana kilipomaliza ziara ya kujiimarisha na kukagua utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya mwaka 2010.
Pia, ziara hizo ziligongana na zile za Chama cha ACT - Wazalendo zilizosababisha Chadema na chama hicho kipya kugongana Butiama.

1 comment:

  1. Mimi nawaunga mkono UKAWA kwa juhudi na mpango wao wa kuungana.Katika dunia ya sasa viongozi/watu wanaungana kwa masirahi ya kuijenga nchi yao,pamoja na kufungua milango ya kidemokrasia ili kila mtu mwenye uwezo aweze kushiriki katika uongozi au nafasi ya kulitumikia taifa lake.Kwa mifumo ya demokrasia tuliyonayo hairuhusu kabisa kila mtanzania kushiriki kirahisi katika uongozi wa nchi hii.Ukiangalia hasa katika kipindi cha chama kimoja, mgombea mmoja na upande mwingi hakuna mtu wa kushindana naye.sio kwamba kulikuwa hakuna watanzania wenye uwezo wa kuongoza nchi.Ukiangalia staili hii bado ipo ndani ya CCM, watu wengine wamekatwa majina yao hata hawapewi muda wa kujieleza.Pengine wangejieleza matokeo yangekuwa tofauti.
    Ukiangalia demokrasia za wenzetu walioendelea wanaangalia uwezo wa mtu wa kulitumika taifa lake wala si anatoka chama gani.Kwa hiyo tunao watu wenye uwezo mkubwa lakini nafasi za kutumika hakuna zimeshikiliwa na watu wachache wakisema ndiyo ni ndiyo hapana ni hapana.

    ReplyDelete