TAREHE 06 MEI 2015
Rais wa
Shirikisho la Mpira wa Miguu DunianI - FIFA, Joseph Blatter ametuma
salamau za pongezi kwa Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini TFF,
Jamal Malinzi kufuatia klabu ya Young Africans kutwaa Ubingwa wa Ligi
Kuu ya Vodacom msimu wa 2014/2015.
Katika
salamu hizo za Blatter, amemuomba Rais wa TFF kufikisha salamu zake za
pongezi kwa klabu ya Young Africans, wanachama, wapenzi wa mpira wa
miguu kwa kupata nafasi ya kuiwakilisha nchi mwakani katika michuano ya
kimataifa barani Afrika.
Blatter
amesema anatambua mafanikio hayo ya kutwaa Ubingwa, yametokana na na
jitihada za uongozi, wachezaji, bechi la ufundi, madaktari, wanachama ,
washabiki na kila mmoja aliyeshiriki katika kufanikisha kutwaa Ubingwa
huo.
Mpira wa
miguu unapata mafanikio makubwa kwa kuvuka mipaka hadi kuwa kichochezi
halisi cha maendeleo, unawasaidia wachezaji wa ngazi zote kuinua vipaji
vyao na mbinu katika kuelekezwa na kubadilika wakati huo huo wakiwa
wakiwa na nyoyo za ushirikiano.
Aidha
Blatter amesema mpira wa miguu kwa sasa ni shule kwa maisha, vijana wa
leo wanaweza kufaidika kupitia kucheza mpira wa miguu kwa ngazi ya
kijamii na mtu mwneyewe binafsi, ndio maana amewapa salamu za pongezi
Young Africans na kuendeleza kazi yao na kuongoza njia ya mafanikio.
Kujituma
kwa klabu ya Young Africans kumewasaidia kushinda Ubingwa huu ikiwa ni
ni mara ya 25, huu ni ushindi mkubwa katika mpira wa miguu.
IMETOLEWA NA SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF)
Attachments area
No comments:
Post a Comment