KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

May 25, 2015

MWIGULU NCHEMBA AJIUZULU NAFASI YA UNAIBU KATIBU MKUU CCM ILI KUWANIA URAIS

Mwigulu Nchemba                                                                                
ALIYEKUWA Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Mwigulu Nchemba amejiuzulu nafasi hiyo ili awanie nafasi ya kugombea urais na nafasi yake imechukuliwa na Rajab Luhavi aliyekuwa mshauri wa rais katika siasa.
Mwigulu amabye pia ni Naibu Waziri wa Fedha, ametangaza kujiuzulu nafasi hiyo leo jioni katika Kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM mkoani Dodoma.
Akithibitisha taarifa hiyo, Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye amesema kuwa Mwigulu ameamua kujiuzulu nafasi hiyo kutokana na nia yake ya kutaka kuomba kuwania urais kwa tiketi ya CCM katika Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Oktoba mwaka huu.
"Mwigulu alikuwa ameshamwambia nia hiyo Mwenyekiti wa Chama, Rais Jakaya Kikwete, naye akamkubalia, sasa leo katika kikao ameomba rasmi kujiuzulu na mwenyekiti amemkubalia mbele ya wajumbe wa NEC" Alisema Nape.
Nape amesema kufuatia uamuzi huo, Mwenyekiti wa CCM, Rais Kikwete amemteua msaidizi wake katika masuala ya siasa, Ndugu Rajabu Ruhavi kuwa Mjumbe wa NEC, na wakati huohuo kumteua kuwa Naibu Katibu Mkuu wa CCM kushika nafasi iliyoachwa na Mwigulu.

No comments:

Post a Comment