Mtu tajiri barani Afrika Aliko
Dangote amesema kuwa bado anataka kuinunua kilabu ya Arsenal licha ya
kushindwa kufanya hivyo mwaka 2010 alipotaka kununua hisa za kilabu
hiyo.
Bilionea huyo kutoka Nigeria ni tajiri mara nane ya
alivyokuwa wakati alipojaribu kununua hisa za klabu hiyo na kwamba
shabiki huyo wa Arsenal bado hajatupilia mbali ndoto yake ya kutaka
kuinunua kilabu hiyo ya Landon Kazkazini.''Bado nina matumaini kwamba siku moja nitainunua timu hiyo',' alisema Dangote mwenye umri wa miaka 58.''Naweza kuinunua bei ambayo wamiliki wake itakua vigumu kukataa'', huku akiongezea kuwa ''najua mpango wangu''.
No comments:
Post a Comment