KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

June 27, 2015

CHADEMA YATOA SALAAM ZA RAMBI RAMBI KUFUATIA MSIBA WA EDSON KAMUKARA




Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimepokea kwa mshtuko na majonzi makubwa kifo cha aliyekuwa mmoja wa waandishi wa habari mahiri na mhariri wa gazeti la mtandaoni, Mwanahalisi Online, Edson Kamukara, kilichotokea ghafla jana jioni katika mazingira yanayodaiwa kuwa ni ajali ya moto.
Kumwelezea Edson Kamukara ambaye kabla ya kuhamia Mwanahalisi Online linalomilikiwa na Hali Halisi Publishers, alikuwa Mhariri wa Gazeti la Tanzania Daima, akiwa ametokea Gazeti la Jambo Leo ambalo alijiunga nalo akitokea Gazeti la Majira, katika nafasi hii ya salaam za pole yenye ukurasa mmoja, linaweza kuwa jambo gumu sana.
Marehemu Kamukara alikuwa mmoja wa waandishi makini na mahiri ambao tasnia ya habari ingeweza kujivunia kuwa nao (wakiwa hai) kwa muda mrefu, hususan katika changamoto kadhaa ambayo taaluma hiyo adhimu inapitia kwa sasa nchini Tanzania.

No comments:

Post a Comment