KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

June 26, 2015

MAKAMU WA RAIS WA BURUNDI AKIMBIA NCHI

Gervais Rufyikiri
Gervais Rufyikiri
 Mmoja wa Makamu wa Rais  Burundi ameikimbia nchi yake baada ya kudai kutishwa kufuatia hatua yake ya kumpinga Rais Pierre Nkurunziza kuongeza muhula wa tatu 

Burundi iko kwemye  machafuko  tangu Rais Nkurunziza alipotangaza  kwania muhula wa tatu kwenye uchaguzi utaofanyika julai mwaka huu
Gervais Rufyikiri aliiambia France24 TV kwamba kuongeza muhula watatu sio katiba inavyoeleza

Msemaji wa serikali  alikanusha kwamba Rufyikiri alitishiwa maisha
 Kuna taarifa kuwa Spika Mhe. Pie Ntavyohanyuma amekimbilia Ubelgiji akidai kuwa ameenda kutibiwa naye  alimpinga Rais kugombea muhula wa tatu
Wote wawili wana uraia wa Ubelgiji.

Maandamano ya kumpinga yalinza Bujumbura baada ya Nkurunziza  kutangaza kwamba atagombea muhula wa tatu

No comments:

Post a Comment