KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

June 11, 2015

OFISI YA TAIFA YA UKAGUZI YAENDESHA MAFUNZO KWA TAASISI WADAU WA USIMAMIZI WA SHERIA

Displaying IMG_5858.JPG
Afisa Sheria wa NAOT, Bw. Frank Sina (kulia) akizungumza katika mafunzo hayo.                         
Na Mwandishi wetu
Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi imeendesha mafunzo ya siku moja ya Taasisi Wadau wa Usimamizi wa Sheria juu ya Ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu  za Serikali (CAG) na jinsi ya kuitafsiri yanayofanyika katika Hoteli ya Den France jijini Dar es Salaam.
Akizungumza wakati akifungua mafunzo hayo, Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Prof. Mussa Assad alisema kuwa mafunzo yanalenga kuwapa ufahamu juu ya ripoti za ukaguzi ambazo Ofisi yake inazitoa, na jinsi ya kuzitafsiri na kushughulikia masuala ya maadili yanatokana na ripoti za ukaguzi.
Prof. Assad aliongeza kuwa mafunzo hayo yanafanyika kwa kuzingatia Kifungu cha 27 cha Sheria ya Ukaguzi wa Umma, 2008, kama ilivyofanyiwa mabadiliko na Sheria ya Fedha Na. 10 ya mwaka 2010.
Kwa mujibu wa kifungu hiki, kinawataka wakaguzi wanaofanya kazi kwa niaba ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali mara tu wanapobaini kuwepo kwa viashiria vya ulaghai/kugushi au rushwa wanapokuwa wanafanya ukaguzi kutoa taarifa kwa CAG.
Kifungu kinaongeza kuwa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali akithibitisha kuwepo wa viashiria hivyo anapaswa mara moja kuvitaarifu vyombo vya dola vya uchunguzi na nakala ya taarifa hiyo kuiwasilisha kwa Mkurugenzi wa Mashitaka.
“Kifungu hiki kinaeleza vyombo hivyo vya dola (DCI/PCCB) kufanya uchunguzi wa kitaalamu juu ya tuhuma hizo na kukamilisha zoezi la uchunguzi ndani ya siku 60 tangu siku ya kwanza. Mara baada ya kumaliza uchunguzi huu vinapaswa kuwasilisha ripoti yao kwa Mkurugenzi wa Mashitaka kwa ajili ya maamuzi ya hatua za kisheria zinazopaswa kuchukuliwa. Mkurugenzi wa Mashitaka anapaswa kwa mujibu wa kifungu hiki kumtaarifu Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu juu ya hatua alizochukua,” Prof. Assad alifafanua.
Displaying IMG_5868.JPG
Mkurugenzi Msaidizi wa Mafunzo, Bibi Felista Tirutangwa (aliyesimama) akizungumza wakati wa kumkaribisha Mgeni Rasmi, Mthibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), wakati wa Ufunguzi wa Mafunzo ya Taasisi Wadau wa Usimamizi wa Sheria Juu ya Ripoti ya Ukaguzi ya CAG na Jinsi ya Kuitafsiri yaliyofanyika katika Hoteli ya Den France, Dar es Salaam.              
Displaying IMG_5875.JPG
Washiriki wa Mafunzo ya Taasisi Wadau wa Usimamizi wa Sheria Juu ya Ripoti ya Ukaguzi ya CAG na Jinsi ya Kuitafsiri wakimsikiliza kwa makini Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG),  Prof. Mussa Assad (aliyesimama). Mafunzo hayo yalifanyika katika Hoteli ya Den France, Dar es Salaam.               

No comments:

Post a Comment