KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

July 30, 2015

SERIKALI YATAKIWA KUANZISHA KITENGO CHA IDARA YA MIKOPO MKOA WA KASKAZINI UNGUJA

03
Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini  Unguja.

……………………………………………………………………………..

Na Maryam Kidikona Miza Kona –Maelezo Zanzibar 

Serikali imetakiwa kuanzisha  kitengo cha Idara ya Mikopo katika Mkoa wa Kaskazini  Unguja ili kuwaondosha usumbufu wananchi wanapotakata kurejesha  fedha za mikopo waliochukua.

Akizungumza na waandishi wa habari Afisa wa Vyama vya Ushirika Wilaya ya Kaskazini ‘A’ Faki Khamis Makame  Ofisini kwake Gamba amesema wanavikundi waliochukua mikopo kwa ajili ya kuendeleza  vikundi vyao wanapata usumbufu wakati wanapotaka kurejesha mikopo hiyo kwa wakati.

“Kuna malalamiko kutoka  Idara ya Mikopo kuwa wanavikundi kutoka vijijini hawarejeshi mikopo kwa muda uliopangwa, tatizo  katika Mkoa huu hakuna kitengo cha Idara ya Mikopo kwa ajili ya kukusanya  mikopo hiyo  hivyo inakuwa usumbufu kwa wanavikundi   kutumia gharama kubwa kuliko pesa wanazozirejesha,” ameeleza Afisa huyo.

Alisema  kutokana na tatizo hilo inakuwa vigumu kurejesha mikopo yao kwa wakati na kuitaka Idara  ya mikopo kuweka mwakilishi wa kukusanya marejesho ya  mikopo yao ndani ya Wilaya hiyo.

Afisa huyo wa Vyama vya Ushirika alifahamisha kuwa kuwepo kwa kitengo hicho Wilayani kutasaidia kupatikana kwa urahisi huduma hiyo pamoja na kuondosha usumbufu uliopo katika Mkoa wao.

Alieleza kuwa tatizo la usafiri kwa wanavikundi ni changamoto kubwa inayorejesha  nyuma maendeleo na juhudi wanazochukua  katika kujikwamua na umasikini ndani ya  Mkoa huo.

Wakati huo huo Afisa huyo wa Vyama vya Ushirika amewataka wanachma wa Vyama hivyo kufanya uchaguzi ndani ya vyama vyao ili kupata viongozi waliobora wenye uwezo wa kuviendeleza vikundi hivyo.

Amesema sula la kuwa na viongozi wenye uwezo wa kuviendeleza vikundi vyao, maendeleo ya haraka yanaweza kufikiwa kwa kipindi kifupi.

“Nawaomba wanaushirika mufanye uchaguzi ili kupata viongozi wazuri watakaoweza kuhifadhi kumbukumbu na kuweka vyema hisabu katika vyama vyenu,”Alisema Afisa Ushirika .

Amewapongeza akinamama wa Wilaya hiyo kwa kuwa mstari wa mbele kuanzisha  na kujiunga  na vyama vya Ushirika ambavyo vimekuwa mkombozi kwao na kuachana  na ile  tabia iliyozoelekea yakuwa tegemezi kwa waume zao.

No comments:

Post a Comment