KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

August 14, 2015

POLISI WAMZUIA LOWASSA KUZIKA



MMGL0471

MGOMBEA urais wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Edward Lowassa, amepata kashikashi baada ya polisi kumzuia kumzika mwasisi wa Chama cha TANU na CCM, Peter Kisumo, kwa madai kuwa wamepata maagizo kutoka juu.

Msafara wa Lowassa ulioanzia Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA), ulikutana na kizuizi cha polisi katika Kijiji cha Maroro, kilomita moja kutoka Mwanga kuelekea Ugweno, ambako Kisumo alizikwa jana.

Lowassa akiongozana na viongozi mbalimbali, akiwamo Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi, James Mbatia, Mwenyekiti wa Chadema Kilimanjaro, Philemon Ndesamburo na Mbunge wa Vunjo, Augustine Mrema, walikuwa na msafara wa magari na pikipiki zaidi ya 100.

Licha ya kwamba msafara wa kiongozi huyo ulitoka KIA ukiwa na magari machache, idadi ya magari na pikipiki iliongezeka kadiri safari ilipokuwa ikiendelea kutokana na baadhi kujiunga kila alipokuwa akipita.

KIZUIZI
Akizungumza na waandishi wa habari waliokuwapo kwenye msafara huo, Mbatia alisema kuwa alizungumza na Mkuu wa Jeshi la Polisi, IGP Ernest Mangu na akawaruhusu kuendelea na safari, lakini Mkuu wa Polisi Mwanga alikataa kutii agizo hilo.

“Nimeongea na IGP akiwa Kibondo, tukakubaliana na kutoa maelekezo kwa RPC, lakini tuliporuhusiwa na kuanza kuondoka, ikaja amri kutoka kwa OC CID akiwa huko juu msibani, ya kwamba hakuna kuruhusu msafara huo, kama kupanda ni gari moja tu la Lowassa na langu,” Alisema Mbatia na kuongeza.

“Lowassa ni Waziri Mkuu mstaafu, huwezi kusema eti iende gari moja tu, na pia siye viongozi wengine wanatunyima haki yetu.
“CCM sasa wameamua kuipasua nchi, Serikali ya CCM inatupeleka kwenye hali ya kutozikana, wametuzuia kwenda kumzika mzee wetu Kisumo, kisa woga tu.”

Wakati yote hayo yakiendelea, Lowassa na  Ndesamburo, walikuwa kwenye magari.

Lakini hata hivyo, baada ya mazungumzo ya muda mfupi, hatimaye majira ya saa 6:53 mchana, msafara huo uliofika eneo hilo saa 6:42, uliruhusiwa kuendelea na safari wakitakiwa kuondoa bendera za Chadema kwenye magari na pikipiki.

MTANZANIA

No comments:

Post a Comment