KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

October 4, 2015

BREAKING NEWS:KINGUNGE AJITOA CCM, ASEMA CCM IMEISHIWA PUMZI YA KUONGOZA


Mzee Kingunge Ngombale Mwilu(Pichani) amesema kuwa hakubaliani na yaliyotokea mjini Dodoma wakati wa kumpitisha Dkt.Magufuli na kilichotokea ni kuwadhalilisha wagombea. Alisema Kamati Kuu ilipaswa kuwahoji "Hilo halikufanyika na wamewadhalilisha na kuwazungusha chini nzima kutafuta wadhamini lakini hilo halikufanyika. Anasema Katiba  ya CCM inasema binadamu wote ni sawa na Binadamu wanastahili heshima" Kuwasumbua wazunguke na kisha kuwafungia milango siyo kuwadhalilisha?"

Amesema kwa bahati mbaya hata viongozi hawajui haki zao na hata wakizijua hawana ujasiri wa kuzitetea.

“Baadhi yetu tuliingia TANU si kwa kutafuta fedha au vyeo ..sisi wengine katika chama tulitafuta jambo lingine ,tulitafuta ukombozi wa Waafrika,” alisema.

Uongozi wa sasa wa CCM umeamua kukibinafsisha Chama kwa maslahi ya asiyejulikana mambo yanayofanyika ni ya ajabu.

Alisema vijana wanatumiwa kudhalilisha watu wazima, mavuvuzela wanaajiriwa kuwatukana watu,na kwamba hicho si chama walichoshirikiana kukijenga.

Alisema kuanzia leo anaachana na chama na kwamba hawezi kukubali kuwa kenye chama kisichokubali fuata Katiba.

“Sasa nasema kuanzia sasa mimi najitoa kwenye chama cha Mapinduzi,najua uamuzi wangu utawasubua baadhi ya ndugu zangu na jamaa zangu”

Anasema ameshiriki kukijenga na katika kuhakikisha kuwa chama kinakuwa na demokrasia halafu chama kinavunja katiba.

Amesema kuwa hakusudii kujiunga na chama chochote,kwani amekuwa mwanaharakati kwa miaka 61.

Amesema kuwa wananchi wengi hivi sasa wanataka mabadiliko, anasema kuwa hata alivyokuwa Arusha wakati Mgombea wa Ukawa Edward Lowassa anatangaza nia, alisema CCM lazima impe ridhaa mtu anayekubalika na wananchi wengi.

Amesema kwamba kama kila mtu anataka mabadiliko lazima kuna sababu.

“Hata mimi nataka mabadiliko,” alisema.

Alirejea historia ndefu ya namna nchi ilivyokuwa ndani ya Chama kimoja na baadaye mfumo wa vyama vingi. Amesema tangu Rais Jakaya Kikwete achukue nchi uchumi umedumaa.



No comments:

Post a Comment