KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

October 8, 2015

MAGUFULI AZIDI KUIBOMOA CHADEMA KILIMANJARO,AWATOLEA UVIVU WATENDAJI WA SHIRIKA LA UMEME NCHINI

 Mgombea Urais wa CCM Dkt John Pombe Magufuli akimnadi mgombea Ubunge wa jimbo la Moshi mjini Ndugu Davis Mosha kwenye mkutano wa hadhara wa kampeni uliofanyika kwenye uwanja wa Mashujaa,mkoani Kilimanjaro jioni ya leo.PICHA ZOTE NA MICHUZI JR-KILIMANJARO.
 Mgombea wa urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia CCM Dk. John Pombe Magufuli na mgombea ubunge wa jimbo la Moshi mjini Ndugu Davis Mosha wakimsikiliza Bw. Lema aliyekuwa Katibu wa Chadema wilaya ya Hai wakati alipojiunga na CCM katika mkutano huo.

 Mgombea Urais wa CCM Dkt Jonh Pombe Magufuli akimnadi mgombea Ubunge wa CCM ndani ya jimbo la Arumeru Mashariki,ndugu John Daniel Pallangyo,kweye mkutano wa kwampeni uliofanyika katika uwanja wa Ngareselo (USA River),jijini Arusha.

 Mmoja wa wajumbe wa timu ya ushindi ya kampeni za CCM,Dkt Emmanuel Nchimbi akimnadi Mgombea Urais wa CCM Dkt John Pombe Magufuli,kweye mkutano wa kampeni uliofanyika katika uwanja wa CCM,Sanya Juu,mkoani Kilimanjaro.
 Mgombea Urais wa CCM Dkt John Pombe Magufuli akimnadi mgombea Ubunge wa jimbo la Siha,Ndugu Aggrey Mwanri mbele ya wakazi wa Siha (hawapo pichani),waliokuwa wamekusanyika katika uwanja wa CCM kwenye mkutano wa kampeni

Sehemu ya Umati wa Wananchi wa mji wa moshi waliofika katika viwanja vya mashujaa wakimsikiliza Mgombea Urais wa CCM Dkt John Pombe Magufuli,leo jioni kwenye mkutano wa kampeni,mkoani Kilimanjaro.
Magufulika Style  inavyozidi kushika kasi,Davis Mosha mgombea ubunge jimbo la Moshi mjini na madiwani wa Moshi mjini wakimagufulika jukwaani kuonyesha ukakamavu wao.
 Sehemu ya Umati wa Wananchi wa mji wa moshi waliofika katika viwanja vya mashujaa wakimsikiliza Mgombea Urais wa CCM Dkt John Pombe Magufuli,leo jioni kwenye mkutano wa kampeni,mkoani Kilimanjaro.

Katika mkutano wake wa Moshi mjini Dkt. Magufuli amewaonya watendaji wa Shirika la Umeme nchini TANESCO na kuwaambia kama wanazima umeme makusudi ili kuwafanya wananchi waichukie serikali wanafanya makosa na ole wao kwa vitendo hivyo visivyo vya kistaarabu, Amewaambia kwamba bado siku 17 za kampeni akichaguliwa na wananchi na kuapishwa kuwa Rais atawashughulikia ipasavyo kwani  wanajulikana.  “Katika siku hizi zilizobaki watubu wafanye kazi usiku na mchana ili umeme upatikane bila kukatika na kuleta adha kwa wananchi vinginevyo akiingia Ikulu atalala nao mbele”,alisema Dkt Magufuli huku uwaja mzima ukilipukwa kwa mayowe.
 Sehemu ya Umati wa Wananchi wa mji wa moshi waliofika katika viwanja vya mashujaa wakimsikiliza Mgombea Urais wa CCM Dkt John Pombe Magufuli,leo jioni kwenye mkutano wa kampeni,mkoani Kilimanjaro.
  Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano kwa tiketi ya chama cha Mapinduzi CCM Dkt John Pombe Magufuli akisisitiza jambo alipokuwa akihutubia umati wa Wananchi wa mji wa moshi waliofika katika viwanja vya mashujaa Kumsikiliza alipokuwa akijinadi na kuwaga sera zake katika kuomba kura za kuwania nafasi ya Urais kwa kipindi cha awamu ya tano,kwenye uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 25 mwaka huu.

No comments:

Post a Comment