KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

November 29, 2015

DODOMA WAANZA USAFI WA MAZINGIRA

Katibu Tawala wa Mkoa wa Dodoma Ndg. Rehema Madenge (kulia walioingia mtaroni) na watumishi wengine wa ofisi ya Mkuu wa Mkoa wakishiriki zoezi la kusafisha mitaro ya maji ya mvua eneo la Bahi Road mapema leo ikiwa ni mwanzo wa utekelezaji wa agizo la Mhe. Rais la kutumia siku ya uhuru 9 Disemba kufanya usafi wa mazingira.
Watumishi wa Manispaa ya Dodoma wakishiriki zoezi la kufanya usafi kwa kufyeka magugu eneo la makaburi ya Bahi Road mapema leo ikiwa ni mwanzo wa utekelezaji wa agizo la Mhe. Rais la kutumia siku ya uhuru 9 Disemba kufanya usafi wa mazingira.
Wafanyakazi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma na Tume ya Maendeleo ya Ushirika wakijiorodhesha baada ya kumaliza zoezi la usafi wa mazingira mapema leo ikiwa ni mwanzo wa utekelezaji wa agizo la Mhe. Rais la kutumia siku ya uhuru 9 Disemba kufanya usafi wa mazingira, orodha hiyo itatumika kuwabaini watumishi ambao hawajashiriki zoezi la usafi.

No comments:

Post a Comment