KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

November 24, 2015

KIPINDUPINDU CHAPUNGUA DAR

index

Na Jacquiline Mrisho- maelezo
 Idadi ya wagonjwa wa kipindupindu jijini Dar es salaam imepungua kufikia wagonjwa kumi na mbili (12) kwa mkoa mzima, huku wilaya ya Temeke ikiwa na wagonjwa saba,Kinondoni wagonjwa wanne na Ilala ikiwa na mgonjwa mmoja
.
Haya yamezungumzwa na Mratibu wa Magonjwa  ya kuambukiza wa Jiji la Dar es salaam  Bw. Alex Mkamba ofisini kwake leo akielezea jinsi gani mkoa umefanikisha kupambana na kipindupindu kwa kuzingatia usafi katika jiji.
Ameongeza kuwa katika kufanikisha mapambano dhidi ya kipundupindu wametoa mafunzo  juu ya mbinu shirikishi ya namna ya kujikinga na kipindupindu kwa watendaji wa mitaa na pia imewahimiza kukagua maeneo yao na kuwapa kibali cha kufunga maeneo ya biashara au maeneo yatoayo huduma za chakula  yasiyozingatia usafi.
Akielezea kuhusu huduma kwa wagonjwa wa kipindupindu jijini  Dar es salaam mratibu huyo amesema jiji lina dawa za kutosha za kuhudumia wagojwa ipasavyo  kwa kuwapatia huduma bora zaidi kuendana na kasi ya maambukizi yaliyopo.
“ hata leo Shirika la Afya Duniani (WHO) limetoa dawa za kusafishia maji (Water Guard) maboksi 45 kwa kila wilaya” Mkamba alifafanua.
Aidha alisema serikali imejipanga katika kudhibiti maambukizi mapya kwa kuwapima wagonjwa kabla na baada ya kuruhusiwa kutoka hospitalini  na aliwashauri wananchi kubadili tabia kwa kuhakikisha usafi unafanyika pia  kuchemsha maji na kuufanya usafi kuwa ni tabia yao ya kila siku.
Mpaka sasa jumla ya watu 55 wamefariki dunia kwa ugonjwa wa kipindupindu jijini Dar es salaam.

No comments:

Post a Comment