KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

December 5, 2015

MKURUGENZI MKUU NHC AZUNGUMZIA UMUHIMU WA MIKOPO YA NYUMBA KONGAMANO LA WAHANDISI

Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Nehemia Kyando Mchechu akizungumza kwenye kongamano la 28 la Taasisi ya Wahandisi Tanzania (Institution of Engineers Tanzania – IET) juu ya mchango wa sekta ya fedha na mikopo ya nyumba katika kuimarisha sekta ya ujenzi wa nyumba endelevu za gharama nafuu nchini. Kongamano hilo linalofanyika kwa siku mbili jijini Dar es Salaam linafanyika kwenye Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Mwalimu Julius Nyerere. IET ni Taasisi inayojitegemea iliyoundwa mwaka 1977, ikiwa na lengo la kuimarisha fani ya Uhandisi hapa nchini. Taasisi hii tayari ina jumla ya wanachama 3,000 kutoka katika sekta mbalimbali hapa nchini.

No comments:

Post a Comment