MKUTANO WA 10 WA UHAMAJI KUTOKA MFUMO WA ANALOGIA KWENDA DIGITALI KWA NCHI ZA SADC WAHITIMISHWA JIJINI DAR ES SALAAM.
Mkurugenzi
wa Idara ya Habari (MAELEZO) na Msemaji wa Serikali Bw. Assah Mwambene
akifunga Mkutano wa 10 wa uhamaji kutoka mfumo wa Analogia kwenda
Digitali kwa nchi za Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za
Kusini mwa Afrika (SADC) kwa niaba ya Katibu Mkuu, Wizara ya Habari,
Vijana Utamaduni na Michezo jana. Tanzania imepata heshima ya kuwa
mwenyeji wa mkutano huo baada ya kuonekana kufanya vizuri katika
uhamaji wa matumizi ya mfumo wa analogia kwenda digitali kwa wakati.
Mkurugenzi
wa Idara ya Habari (MAELEZO) na Msemaji wa Serikali Bw. Assah Mwambene
(katikati) akiwaonesha jambo kupitia Kitumi chake cha Mkononi (IPAD)
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Dkt. Ally
Simba (kulia) na Naibu Mkurugenzi wa Utangazaji wa Mamlaka ya
Mawasiliano Tanzania(TCRA) Bw. Fredrick Ntobi (kushoto) kabla ya kufungwa kwa Mkutano wa 10 wa uhamaji kutoka mfumo wa Analogia kwenda Digitali kwa nchi za Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC) jijini Dar es salaam.
Washiriki wa Mkutano wa 10 wa uhamaji kutoka mfumo wa Analogia kwenda Digitali kwa nchi za Jumuiya
ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC) wakifuatilia masuala
mbalimbali wakati wa mkutano huo jijini Dar es salaam.
Mada mbalimbali zikiwasilishwa kwa washiriki wakati wa Mkutano wa 10 wa uhamaji kutoka mfumo wa Analogia kwenda Digitali kwa nchi za Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC) jijini Dar es salaam.Picha Aron Msigwa – MAELEZO.
No comments:
Post a Comment