KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

February 10, 2016

SERIKALI KUMALIZIA DENI LA MAKANDARASI BILIONI 800 IFIKAPO JUNI MWAKA HUU

MRW
Na Lorietha Laurence-Maelezo
Serikali imedhamiria kumalizia deni la Makandarasi la kiasi cha zaidi ya bilioni 800  ifikapo Juni mwaka huu ambapo tayari kiasi cha bilioni 400 zimeshalipwa katika kufanikisha ujenzi wa barabara za ndani ya jiji la Dar es Salaam
Hayo yamesemwa na Waziri wa Ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano  Prof.Makame Mbarawa wakati wa ziara yake ya kukagua ujenzi wa barabara hizo leo jijini Dar es Salaam lengo ikiwa ni kupunguza msongamano katika njia kuu.
“Lengo la Serikali ni kuhakikisha kuwa  inapunguza msongamano na hivyo kuwarahisishia wananchi wake usafiri , kukamilika kwa ujenzi huo ni afueni kwa wakazi wa jiji la Dar es Salaam” alisema Prof.Mbarawa.
Aliongeza kuwa ujenzi huo umegharimu kiasi cha shilingi Tilioni 1.2 chini ya ufadhili wa serikali yenyewe kwa asilimia 100 kupitia Bodi ya  Mfuko wa Barabara nchini (RFB)   .
Prof.Mbarawa aliongeza kuwa kumekuwepo na changamoto mbalimbali ikiwemo ujenzi holela  pamoja na ulipwaji wa fidia na kuwaomba wananachi pale wanapofanya ujenzi kujenge mbali na barabara ili kuepeukana na usumbufu wa mara kwa mara.
Naye Mkurugenzi Mkuu waWakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) Patrick Mfugale  ameeleza kuwa tayari baadhi ya wananchi wameshalipwa  fidia kwa wale waliopisha ujenzi katika maeneo ambayo barabara zinatakiwa kupita na hivyo kurahisisha usafirishaji kwa wananchi wake.
“Natoa wito kwa wananchi kutoa ushirikiano kwa kupisha maeneo yale yote yaliyowekewa alama kwa ajili ya ujenzi  ili kukamilisha ujenzi mapema iwezekanayo “ alisema  Mfugale.
Ziara hiyo ya kukagua ujenzi wa barabara za ndani ilianzia katika barabara ya  Tanki Bovu kwenda Goba  kilomita 9.0,baadaye kuelekea ,Mbezi , Malambamawili,Kinyerezi hadi Banana yenye urefu wa  kilomita 14 na Tabata Dampo-Kigogo na ile ya Ubungo Maziwa ,mabibo hadi External kilomita 2.25.
Maradi huo wa ujenzi wa barabara za ndani upo katika awamu mbili huku awamu ya kwanza ya kilomita 27 ikiwa inatarajia kukamilika mwezi Aprili mwaka huu na baadaye kumalizia awamu ya pili ya kilomita 28 tayari kwa kuanza ujezni wa awamu ya tatu barabara ya Goba-wazo hill kilomita 13.0,Mbezi Mwisho Malambamawili –kifuru kilomita 6, na Goba –Makongo-Ardhi kilomita 9.

No comments:

Post a Comment