Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (katikati) akiwa katika moja ya kikao na wakandarasi wanaosambaza Umeme
Vijijini vilivyoanza tarehe 29 Machi na kumalizika tarehe 31 mwezi
huu.Wa Tatu kulia ni Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini
(REA), Dkt. Lutengano Mwakahesya na wa pili kulia ni Mkurugenzi wa Ufundi kutoka
REA, Mhandisi Bengie Msofe. Wengine ni watendaji kutoka kampuni ya
Angelique International inayosambaza umeme mkoani Arusha, Wizara na REA.
Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (katikati) akiwa katika kikao na kampuni ya
Engineering & Construction inayosambaza umeme vijijini mkoani
Kagera katika wilaya za Ngara, Biharamulo, Misenyi, Karagwe, Kyerwa,
Bukoba vijijini na Muleba kilichofanyika katika ukumbi wa Wizara ya
Nishati na Madini jijini Dar es Salaam. Wa kwanza kulia ni Mkurugenzi
Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Dkt. Lutengano Mwakahesya na
anayemfuatia ni Meneja wa Tanesco Kanda ya Ziwa, Mhandisi Amos
Maganga.Wengine ni watendaji kutoka kampuni hiyo, Wizara na REA.
Naibu
Katibu Mkuu, Wizara ya Nishati na Madini, Dkt. Mhandisi Juliana
Pallangyo (wa kwanza kushoto), Meneja wa Tanesco Kanda ya Ziwa, Mhandisi
Amos Maganga (wa pili kushoto), na Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati
Vijijini (REA), Dkt. Lutengano Mwakahesya (wa Tatu kushoto) wakiwa
katika moja ya vikao vilivyojumuisha wakandarasi wanaosambaza umeme
vijijini vilivyoanza tarehe 29 Machi na kumalizika tarehe 31 Machi, mwaka huu.


No comments:
Post a Comment