KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

March 2, 2016

MAMLAKA YA HALI YA HEWA NCHINI TMA, YAWAPIGA MSASA WANAHABARI KUHUSU EL-NINO NA ATHARI ZAKE.


mz
Katibu Tawala Wilaya ya Nyamagana Mkoani Mwanza Marcella Mayalla, akifungua Warsha ya Siku mbili kwa Wanahabari Kuhusu El-Nino na athari zake katika Mvua hapa nchini, iliyofanyika hii leo Jijini Mwanza. Mayalla amefungua Warsha hiyo kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Magesa Mulongo.
…………………………………………………………………………………
Na:George Binagi-GB Pazzo
Katika Warsha hiyo, Taasisi mbalimbali pamoja na Wanajamii, zimehimizwa kutumia taarifa za Utabiri wa Hali ya Hewa kwa ajili ya Mipango ya Maendeleo.
 
Pia Wanahabari ambao ni kiunganishi Muhimu katika upashanaji wa habari, wametakiwa kutumia nafasi yao katika kutoa taarifa hizo kwa wananchi ikizingatiwa kwamba, taarifa za utabiri wa hali ya hewa zikiwafikia walengwa kwa wakati, husaidia kujikinga na maafa yatokanayo na mabadiliko ya tabia nchi ikiwemo Mafuriko na ukame.
 
Warsha hiyo imeandaliwa na Mamlaka ya Hali ya Hewa nchini (TMA), kwa ushirikiano wa karibu na Mamlaka ya Hali ya Hewa Duniani (WMO) ikiwa ni katika mpango wake wa Kidunia katika kuboresha upatikanaji wa taarifa za hali ya hewa ujulikanao kama Global Framework For Climate Services (GFCS).
Katibu Tawala Wilaya ya Nyamagana Mkoani Mwanza Marcella Mayalla, akifungua Warsha ya Wanahabari Kuhusu El-Nino na athari zake katika Mvua hapa nchini, iliyofanyika hii leo Jijini Mwanza. Mayalla amefungua Warsha hiyo kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Magesa Mulongo.
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa nchini (TMA) Dkt.Agness Kijazi akizungumza katika Ufunguzi wa Warsha ya siku mbili kwa Wanahabari Kuhusu El-Nino na athari zake katika Mvua hapa nchini, iliyofanyika hii leo Jijini Mwanza.
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa nchini (TMA) Dkt.Agness Kijazi akizungumza katika Ufunguzi wa Warsha ya siku mbili kwa Wanahabari Kuhusu El-Nino na athari zake katika Mvua hapa nchini, iliyofanyika hii leo Jijini Mwanza.
Kulia ni Meneja wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Kanda ya Ziwa, Augustino Nduganda akitoa neno la Shukrani baada ya Ufunguzi wa Semna kwa Wanahabari Kuhusu El-Nino na athari zake katika Mvua hapa nchini.

No comments:

Post a Comment