KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

March 31, 2016

WAZIRI UMMY MWALIMU AWAKEMEA WANAOJICHUKULIA SHERIA KWA WATUMISHI WA AFYA/


Ummy Mwalimu
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mh. Ummy Mwalimu akizungumza na na watumishi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mtwara Ligula kufuatia tukio la mmoja wa Madaktari kupigwa na mwananchi. Kulia ni Mganga Mkuu wa Serikali Prof. Mohammed Kambi.
………………………………………
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mh. Ummy Mwalimu akemea tabia inayotaka kujengeka ndani ya jamii ya kuwashambulia watumishi wa afya hasa Madaktari na Wauguzi.
Amevitaka vyombo ya dola kuwachukulia hatua wananchi wanaojihusisha na vitendo hivi ambavyo vitaathiri utoaji wa huduma za afya kwa wananchi hasa wa kipato cha chini.
Mhe Ummy amewasili Mtwara jana akiongozana na Mganga Mkuu wa Serikali Prof. Mohammed Kambi ambapo alifanya mazungumzo na watumishi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mtwara Ligula.
Amewaonya wananchi kutoitumia vibaya dhamira ya dhati ya Rais Dkt. John Magufuli na Serikali ya kuimarisha nidhamu na uwajibikaji katika utumishi wa umma kwa kujichukulia sheria mkononi.
Ummy Mwalimu
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mh. Ummy Mwalimu akizungumza na mmoja wa wazee aliyefika kupata matibabu katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mtwara Ligula mara baada kuwasili hospitalini hapo kuzungumza na wafanyakazi.
Ummy Mwalimu
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mh. Ummy Mwalimu akizungumza na baadhi ya wananchi waliokusanyika nje ya hospitali kufuatia tukio la mwananchi kumpiga daktari.
Ummy Mwalimu
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mh. Ummy Mwalimu akisikiliza maoni kutoka kwa mmoja wa wananchi aliyefika hospitalini hapo.
Ummy Mwalimu
Mh. Ummy Mwalimu akizungumza na na watumishi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mtwara Ligula kufuatia tukio la mmoja wa Madaktari kupigwa na mwananchi. Kulia ni Mganga Mkuu wa Serikali Prof. Mohammed Kambi.
Ummy Mwalimu
Baadhi ya watumishi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mtwara Ligula wakimsikiliza Mh. Ummy Mwalimu (hayupo pichani).

No comments:

Post a Comment