KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

April 4, 2016

F KLSA ASSOCIATES YAJIUNGA NA PKF, PROF. ASSAD AWATAKA KUONYESHA UBORA ZAIDI

DSC_0122Katika kuhakikisha wanajitanua katika utoaji wa huduma bora za uhakiki na ukaguzi wa hesabu, kampuni ya KLSA Associates ya nchini imejiunga na mtandao wa kimataifa wa makampuni ya hesabu za kifedha na ushauri ya PKF ambapo baada ya kujiunga imebadilika jina kutoka KLSA Associates na kuwa PKF Associates Tanzania.
Akizungumza katika halfa ya KLSA kujiunga PKF, Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Prof. Mussa Assad aliwapongeza KLSA kujiunga na PKF na kuwataka kuongeza juhudi na kuboresha huduma zaidi kwa kuzingatia kwa sasa wamejiunga na kampuni ambayo inasifika duniani katika ukaguzi wa hesabu, utunzaji wa hesabu za kifedha, ufumbuzi na ushauri wa masuala ya kodi na kibiashara.
“Tunafahamu jinsi PKF wanavyofanya kazi, mmepata nafasi ya kujiunga nao na itarahisisha kwenu kupata hata taarifa nyingi hivyo ni wakati wa kuonyesha kuwa ninyi ni bora katika kutoa huduma,” alisema Prof. Assad.
 Nae Meneja Mshirika wa PKF Associates Tanzania, Mustasir Gulamhussein alisema wameamua kujiunga na PKF kwa kutambua uwezo wao wa kufanya kazi katika maeneo mbalimbali duniani na wanaamini kujiunga kwao kutawawezesha kujitanua katika utoaji wa huduma bora zaidi kutokana na kuwa na wafanyakazi walio na uwezo.
“PKF ni jina linaloheshimika na kutambulika katika uhifadhi wa taarifa za kifedha ulimwenguni na kwa kuwepo Tanzania kunadhihirisha umuhimu wake katika kuwahudumia wateja ambao wanapanua wigo wao kimataifa na tunaamini tutakuwa zaidi katika kutoa huduma,” alisema Gulamhussein.
Kwa upande wa Mkurugenzi wa PKF Kanda ya Afrika, Theo Veemark alisema KLSA ni kampuni nzuri katika utendaji wao wa kazi za uhakiki na ukaguzi wa hesabu hapa nchini na wanaamini kufanya kazi na KLSA kutawawezesha kutanua huduma zao zaidi na kurahisisha utendaji wa kazi.
“Tunafuraha kuwakaribisha KLSA katika familia ya PKF tunaamini kupitia muungano huu tutaweza kutanua soko letu la kibiashara na kubadilishana mawazo ili tuweze kuboresha huduma zetu zaidi,” alisema Veemark.

No comments:

Post a Comment