KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

April 23, 2016

WABUNGE WA EALA-TANZANIA WATEMBELEA CLOUDS MEDIA GROUP




WABUNGE wa bunge la Afrika Mashariki (EALA), kutoka Tanzania, wametembelea Clouds Media Group,Mikocheni jijini Dar es Salaam  Aprili 22, 2016  ikiwa ni sehemu ya ziara yao ya takriban siku 20 kutembelea vyombo vya habari kwa nia ya kuvishirikisha vyombo hivyo kutoa elimu kwa wananchi kuchangamkia fursa zilizopo kwenye Jumuiya ya Afrika Mashariki.
Mkurugenzi wa Vipindi na Uzalishaji wa Clouds Media Group, inayomiliki kituo cha radio, Clouds FM, Clouds TV, Bw. Ruge Mutahaba, amewaeleza wabunge hao walioongozwa na mwenyekiti wao Mh. Chrles Makongoro Nyerere kuwa, Tanzania inakabiliwa na tatizo kubwa la kutogeuza vipaji kuwa biashara na hivyo kujiingizia kipato.
Ruge amewahimiza wabunge hao kushawishi serikali ya Tanzania kurekebisha sera zake za kuwawezesha wananchi na kuwajengea uwezo wa kuvitumia vipaji walivyojaaliwa na Mwenyezimungu ili kujiingizia kipato.
Akielezea nia ya ziara hiyo, Mwenyekii Mh. Makongoro Nyerere alisema, wabunge kutoka nchi wanachama walipewa jukumu la kuwatembelea wananchi wa nchi watokako ili kwahimiza kuchangamkia fursa zilizopo kwenye Jumuiya hiyo ambayo kwa sasa ina jumla ya wanachama sita, Tanzania, Kenya Uganda, Rwanda, Burundi na Sudani Kusini.
“Jumuiya ya Afrika Mashariki ina soko la kutosha na wananchi wa Jumuiya hii wanyo fursa ya kwenda kufanya shughuli za kiuchumi bila kizuizi chochote ikiwemo biashara na kufanya kazi hivyo ni wakati wa watanzania kuacha kulalamika na kuchangamkia fursa hiyo.” Alisema Mh. Makongoro.
Pamoja na Mh. Makongoro, wabunge wengine ni pamoja na Mh. Shy-Rose Bhanji, na Mh. Nderaikindo Kessy.
Imeandaliwa na K-VIS MEDIA/Khalfan Said

Wabunge wa bunge la Afrika Mashariki kutoka Tanzania, na wafanyakazi wa Clouds Media Group, akiwemo mchekeshaji maarufu Bishanga Bashaija, wakiwa kwenye moja ya studio za Clouds Media Group, wakati wa kipindi maarufu cha Leo Tena, Aprili 22, 2016.
Mkurugenzi wa Vipindi na Uzalishaji wa Clouds Media Group, Bw. Ruge Mutahaba, (kulia), akitoa maelezo ya uendeshaji wa kampuni hiyo, wakati wabunge wa bunge la Afrika Mashariki (EALA-Tanzania), walipotembelea studio za Clouds radio/TV Mikocheni jijini Dar es Salaam Aprili 22, 2016. Kutoka kushoto ni Mwenyekiti wa wabunge hao Mh. Charles Makongoro Nyerere, Mh. Nderaikindo Kessy, na Mh. Shy-Rose Bhanji.
Mtangazaji wa kipindi cha Leo Tena, Gea Habib
 Mwenyekiti Mh. Charles Makongozo Nyerere (kulia) akizungumza kwenye kipindi cha Leo tena
Mh. Shy-Rose Bhanji mkutanoni
Mh. Nderaikindo Kessy akiwa mkutanoni
Mtangazaji wa kipindi cha Leo Tena Husna Abdul  “DAHUU”
 Mwenyekiti Mh. Charles Mkongoro Nyerere akizungumza kwenye kikao cha kubadilishana mawazo na uongozi wa Clouds Media Group.
shyrose Bhanji
Mh. Shy-Rose Bhanji, akizungumza kwenye kikao hicho

No comments:

Post a Comment