Klabu ya soka ya Atletico Madrid
imefanikiwa kutinga fainali ya klabu bingwa barani Ulaya kwa mara ya
pili ndani ya kipindi cha miaka mitatu baada ya kupata bao la ugenini
walipokipiga dhidi ya Bayern Munchen ya Ujerumani. Wakiwa na faida ya
bao la nyumbani katika nusu fainali ya kwanza nchini Hispania, Bayern
walisawazisha kupitia mkwaju wa adhabu ndogo uliopigwa na Xabi Alonso.
Mlinda
mlango wa Atletico Jan Oblak aliokoa mkwaju wa penalti uliopigwa na
Thomas Muller kabla ya mshambuliaji Antoine Griezmann kusawazisha na
kuwa 1-1
Robert Lewandowski alifunga bao la pili baada ya kupokea
pasi ya mpira wa kichwa kutoka kwa Arturo Vidal huku Atletico
wakishindwa kusawazisha baada ya mkwaju wa penalti uliopigwa na Fernando
Torres kuokolewa na mlinda mlango Manuel Neuer.
Kwa maana hiyo
Atletico watakutana katika fainali mjini Milan tarehe 28 Mei na mshindi
wa mchezo kati ya Real Madrid na Manchester City utakaopigwa kesho
dimbani Santiago Bernabeu
|
May 4, 2016
ATLETICO MADRID YATINGA FAINALI ULAYA
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment