KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

May 2, 2016

MKUU WA MKOA WA KILIMANJARO ATUNUKU VYETI KWA WASHIRIKI WA KAMPENI YA SIKU 10 YA USAFI KATIKA HIFADHI YA TAIFA YA MLIMA KILIMANJARO (KINAPA)

Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro ,Said Mecky Sadicky akitoa vyeti kwa wawakilishi
wa Kampuni mbalimbali zilizosaidia katika kampeni ya siku 10 ya kufanya
usafi katika Hifadhi ya Taifa ya Mlima Kilimanjaro (KINAPA),Zoezi la
utoaji Vyeti limefanyika katika lango la Marangu wakati wa hafla fupi ya
kuwapokea washiriki wa zoezi hilo la usafi.
Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro ,Said Mecky Sadicky akizungumza na washiriki wa
kampeni ya siku 10 ya kufanya usafi katika Hifadhi ya Taifa ya Mlima
Kilimanjaro (KINAPA) muda mfupi mara baada ya kurejea. 
Baadhi ya Washiriki wa Kampeni ya siku 10 ya kufanya usafi katika Hifadhi ya
Taifa ya Mlima Kilimanjaro wakifuatilia hotuba ya Mkuu wa Mkoa wa
Kilimanjaro Said Mecky Sadicky alipokuwa mgeni rasmi katika Hafla ya
kutunuku vyeti kwa washiriki pamoja na wamiliki wa kampuni.
Mkuu wa Wilaya ya Moshi,Novatus Makunga akizungumza katika Hafla hiyo.

No comments:

Post a Comment