Na. Aron Msigwa – Dodoma.
Mwamko mdogo wa Watanzania
kutembelea hifadhi za Taifa zilizo katika maeneo mbalimbali nchini
umeathiri kiwango cha idadi ya watu wanaotembelea hifadhi hizo kwa mwaka
hivyo kuzorotesha mapato yanayotokana na watalii wa ndani ya nchi.
Kauli hiyo imetolewa Bungeni
mjini Dodoma na Waziri wa Maliasili na Utalii Prof. Jumanne Maghembe
wakati akiwasilisha Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya wizara
hiyo kwa mwaka wa fedha wa 2016/2017.
Amesema kuwa licha ya Serikali
kuweka gharama ndogo za viingilio katika hifadhi za Taifa kwa watanzania
na raia wa Jumuiya ya Afrika Mashariki bado mwamko ni mdogo hasa idadi
ya watanzania wanaokwenda kutembele hifadhi hizo jambo linalopunguza
mapato yanayotokana na utalii wa ndani wa watanzania.
Ameeleza kuwa kwa sasa watanzania
kwa maana ya watu wazima wanaotembelea hifadhi za ndani zilizoko eneo
la Kaskazini hutakiwa kulipa kiingilio cha shilingi elfu kumu
(10,000) na shilingi elfu 5000 hadi 15,000 kwa hifadhi zote zilizoko
kusini mwa Tanzania huku watoto wakilipia shilingi 2000 kutembelea
hifadhi yoyote nchini.
Prof. Maghembe ameeleza kuwa
kufuatia hali hiyo Wizara yake inaendelea na kampeni mbalimbali ili
kuwahamasisha Watanzania Wengi zaidi kushiriki katika shughuli za
utalii ndani ya nchi hivyo kuongeza patoa la Taifa.
Amesema katika kulinda na kutunza
hifadhi za Taifa ili kuhakikisha zinakuwa endelevu na kutoa mchango
mkubwa katika maendeleo ya taifa, Serikali ya awamu ya tano imejipanga
kikamilifu ujangili wa wanyama pori kwa kushirikiana na wadau mbalimbali
wa uhifadhi.
Amefafanua kuwa katika kupambana
na ujangili nchini Wizara kwa kushirikiana na wadau wa uhifadhi
imeshawabaini na kuwashughulikia baadhi ya wananchi wanaoishi kwenye
maeneo yanayopakana na hifadhi wanaoshirikiana na watumishi wasio
waaminifu kushiriki vitendo vya ujangili pia kuwashughulikia wawindaji
haramu wanaojihusisha moja kwa moja kuua wanyama kufanya udalali na
kusafirisha wanyama hao.
Aidha, amesema kuwa katika
kupambana na ujangili Serikali inaendelea kufanya doria ili
kuwashughulikia wawezeshaji ngazi ya nchi wanaonunua nyara, kusambaza
silaha, watakatishaji fedha , majangili nguli wa kimataifa kwa kukitumia
na kukiimarisha kitengo cha Intelijensia ili kiweze kutimiza majukumu
ya kiulinzi kwa ufanisi zaidi.
Pia amesema kuwa Wizara hiyo
imeendendelea kuongeza idadi ya askari wanyamapori 447 na maafisa 111 na
kufanya idadi ya watumishi waliopo kwa sasa kufikia 2,064 pamoja na
kuanzisha kada nane za doria za ushirikiano katika mifumo ya ikolojia ya
Selous-Niassa-Mikumi, Ruaha- Ruangwa, Katavi -Rukwa , Moyowosi -Kigosi,
Tarangire- Manyara-Simanjiro na Ngorongoro – Serengeti.
|
May 24, 2016
MWAMKO MDOGO WA WATANZANIA KUTEMBELEA HIFADHI ZA TAIFA WAATHIRI UTALII WA NDANI.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment