KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

May 24, 2016

MWAMKO MDOGO WA WATANZANIA KUTEMBELEA HIFADHI ZA TAIFA WAATHIRI UTALII WA NDANI.

index
Na. Aron Msigwa – Dodoma.
Mwamko mdogo wa Watanzania kutembelea hifadhi za Taifa zilizo katika maeneo mbalimbali nchini umeathiri kiwango cha idadi ya watu wanaotembelea hifadhi hizo kwa mwaka hivyo kuzorotesha mapato yanayotokana na watalii wa ndani ya nchi.
Kauli hiyo imetolewa Bungeni mjini Dodoma na Waziri wa Maliasili na Utalii Prof. Jumanne Maghembe wakati akiwasilisha Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya wizara hiyo kwa mwaka wa fedha wa 2016/2017.
Amesema kuwa licha ya Serikali kuweka gharama ndogo za viingilio katika hifadhi za Taifa kwa watanzania na raia wa Jumuiya ya Afrika Mashariki  bado mwamko ni mdogo hasa idadi ya watanzania wanaokwenda kutembele hifadhi hizo jambo linalopunguza mapato yanayotokana na utalii wa ndani wa watanzania.
Ameeleza kuwa kwa sasa watanzania kwa maana ya watu wazima wanaotembelea hifadhi za ndani zilizoko eneo la Kaskazini hutakiwa kulipa  kiingilio cha  shilingi  elfu kumu (10,000) na shilingi elfu 5000 hadi 15,000 kwa hifadhi zote zilizoko kusini mwa Tanzania huku watoto wakilipia shilingi 2000 kutembelea hifadhi yoyote nchini.
Prof. Maghembe ameeleza kuwa kufuatia hali hiyo Wizara yake inaendelea na kampeni mbalimbali ili kuwahamasisha Watanzania Wengi zaidi  kushiriki katika  shughuli za utalii ndani ya nchi hivyo kuongeza patoa la Taifa.
Amesema katika kulinda na kutunza hifadhi za Taifa ili kuhakikisha  zinakuwa endelevu na kutoa mchango mkubwa katika maendeleo ya taifa, Serikali ya awamu ya tano imejipanga kikamilifu ujangili wa wanyama pori kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wa uhifadhi.
Amefafanua kuwa katika kupambana na ujangili nchini Wizara kwa kushirikiana na wadau wa uhifadhi imeshawabaini na kuwashughulikia baadhi ya wananchi wanaoishi kwenye maeneo yanayopakana na hifadhi wanaoshirikiana na watumishi wasio waaminifu kushiriki vitendo vya ujangili pia kuwashughulikia wawindaji haramu wanaojihusisha moja kwa moja kuua wanyama  kufanya udalali na kusafirisha wanyama hao.
Aidha, amesema kuwa katika kupambana na ujangili Serikali inaendelea  kufanya doria ili kuwashughulikia wawezeshaji ngazi ya nchi wanaonunua nyara, kusambaza silaha, watakatishaji fedha , majangili nguli wa kimataifa kwa kukitumia na kukiimarisha kitengo cha Intelijensia ili kiweze kutimiza majukumu ya kiulinzi kwa ufanisi zaidi.
Pia amesema kuwa Wizara hiyo imeendendelea kuongeza idadi ya askari wanyamapori 447 na maafisa 111 na kufanya idadi ya watumishi waliopo kwa sasa kufikia 2,064 pamoja na kuanzisha kada nane za doria za ushirikiano katika mifumo ya ikolojia ya Selous-Niassa-Mikumi, Ruaha- Ruangwa, Katavi -Rukwa , Moyowosi -Kigosi, Tarangire- Manyara-Simanjiro na Ngorongoro – Serengeti.

No comments:

Post a Comment