KINSHASA, CONGO: Mwili wa mwimbaji nguli wa muziki wa dansi nchini DR Congo, Papa Wemba, ambao upo ndani ya Nchi hiyo unatarajiwa kuzikwa kijijini kwao keshokutwa siku ya Jumatano ya Mei 4. 2016 tofauti na taarifa ya awali iliyoeleza kuwa nguli huyo angezikwa jioni ya Mei 3.
Modewjiblog kwa mujibu wa taarifa iliyopatikana kutoka katika vyanzo vya habari ikiwemo kurasa wa mtandao wa mwanamuziki huyo, ilitoa taarifa fupi ya ratiba ya maziko hayo na taratibu za kuaga mwili huo.
Leo siku ya Jumatatu Mei 2
  • Kuanzia saa mbili asubuhi mwili utatolewa Hospitali na kuzungushwa katika mitaa ya nchi hiyo na kuelekea katika eneo maalum la kuagia.

  • Kuanzia saa saa nne asubuhi hadi mchana  Rais wa DR Congo, Joseph Kabila ataongoza wananchi wa Congo na wanamuziki kuaga mwili wa Papa na kisha jioni mwilI  huo utapelekwa  kijijini kwa nguli huyo katika kijiji cha Molokai na utalala kijijini kwake.
  • Mei 4.2016 maziko

  • Kwa ratiba hiyo inaonyesha  baada ya mwili huo kulala kwa siku moja katika kijiji cha Papa Wemba na kuendelea na sara na mambo ya mila na kufuatia maziko 

  • Papa Wemba alifariki hivi karibuni jijini Abidjan nchini Ivory Coast ambapo awali alipoteza fahamu akiwa jukwaani alipokuwa akitumbuiza baada ya kuanguka na kukimbizwa hospitali.

  • NB: Modewjiblog itaendelea  kukuletea kila kinachoendelea na endapo ratiba itabadilika tutawajuza pia,..fc99d6_a7e47bd95c2448e59f1bded95baa3da6 fc99d6_460f679d17ef457b8dbb99accac4368c fc99d6_4afe2ba74d1846198ff71cc6af094bb8Pichani ni enzi za uhai wake mwanamuziki Papa WembaDSC_1022Pichani enzi za uhai wake: Mwanamuziki Papa Wemba alipokuja Tanzania, kwenye tamasha la Karibu Music Festival 2015, Bagamoyo-Pwani. Picha na Andrew Chale-Modewjiblog-Bagamoyo).DSC_0825Mwanamuziki Papa Wemba (kushoto) enzi za Uhai wake akipata picha ya ukumbusho na Mwandishi Mwandamizi wa mtandao huu wa Modewjiblog, Andrew Chale wakati wa mahojiano maalum kwenye tamasha la Karibu Music Festival 2015, Bagamoyo Pwani.

  • Mtandao wa MODEWJIBLOG, unatoa pole kwa familia, ndugu, jamaa na marafiki pamoja na wafuasi wote wa mwanamuziki Papa Wemba kwa kuondokewa na kipenzi chao.Nasi tupo pamoja katika kipindi hiki kigumu hivyo tunatoa pole.