KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

July 10, 2016

MWANDISHI WA MAJIRA ELIZABETH MAYEMBA AFARIKI DUNIA

TANZIA: Mwandishi Mwandamizi wa Habari za michezo na burudani wa gazeti la Majira, Elizabeth Mayemba amefariki dunia usiku wa leo baada ya kuanguka ghafla nyumbani kwake eneo la Tabata kwa Swai jijini Dar es Salaam.
Taaifa za awali zinaeleza kuwa, tukio hilo limetokea majira ya saa mbili usiku huu wa Julai 9.2016,ambapo inaelezwa alikuwa akijisikia kizunguzungu na ndipo alipopatwa na umauti huo licha  ya kukimbizwa Hospitali.
Aidha, Taarifa kutoka kwa mume wa marehemu, Eliza, Bwana Rogers amebainisha kuwa…, alipigiwa simu saa mbili usiku na kuambiwa Eliza alisikia kizunguzungu ghafla na kuanguka chini, alichukuliwa na kupelekwa hospital baada muda mtu aliyempeleka Eliza hospital alimpigia tena na kumpa taarifa za Eliza kufariki.
Taarifa nyingine zitatolewa baada ya  ndugu wa marehemu kukutaana. RIP Elizabeth Mayemba.

1 comment:

  1. Nakukumbuka sana mama yangu kipenzi,Mungu akulaze mahali pema peponi

    ReplyDelete