KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

August 22, 2016

POLISI YAKAMATA KIJANA AKIUZA FULANA ZA UKUTA

Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam limesema limejiandaa kudhibiti maandamano ya Umoja wa Kupambana na Udikteta Tanzania (Ukuta) yaliyoandaliwa na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) yanayotarajiwa kufanyika Septemba Mosi mwaka huu.

Wakati akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam, Kamanda wa Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam Simon Sirro amewatoa hofu wakazi wa mkoa huo kuwa hakuna mtu na au kikundi chochote cha watu kitakachofanya maandamano siku hiyo.

“Habari ya Ukuta haipo,umeshabomoka na kama haujabomoka utabomoka, wakazi wa Dar es Salaam msiwe na hofu, fanyeni kazi na hata siku hiyo hakuna mtu atakayejitokeza barabarani kuandamana,” amesema.

Kamanda Sirro amedai kuwa siasa zinatakiwa kufanywa kwa amani na utulivu na kwamba wanasiasa wanaoitumia siasa kufanya vurugu hawatafanikiwa.

“Mimi niwahakikishie kwamba tunajiandaa kwelikweli kuhakikisha watu wanafuata sheria , anayetaka kuvunja sheria kwa kufanya maandamano aanze yeye ili nasi tuanze naye,” amesema.

Ameongeza kuwa ” Suala la utii wa sheria ni la msingi,kama kuna watu au kikundi cha watu kinataka kuitumia siasa kufanya uvunjifu wa amani wajue kwamba nafasi hiyo kwa Dar es Salaam haipo.”

Aidha,Kamanda Sirro amesema August 20 2016 Jeshi la Polisi lilipata taarifa toka kwa raia wema kuwa maeneo ya Kinondoni kuna duka linauza flana zenye maneno ya uchochezi yaliyoandikwa ‘’TUJIPANGE TUKATAE UDIKITETA UCHWARA’’ , ‘UKUTA’ ‘
 
Amesema  Polisi baada ya kupata taarifa hizo walifika eneo la tukio na kumkamata mtuhumiwa aitwaye YORAM SETHY MBYELLAH miaka 42, mfanyabiashara na mkazi wa Mburahati akiwa anauza fulana hizo dukani kwake

2 comments:

  1. This comment has been removed by the author.

    ReplyDelete

  2. TANZANIA: A FAKE CRISIS IN THE MAKING
    With every passing day, Tanzanians wait with bated breath, and some with apprehension, the arrival of September 1. That is the day the main opposition party, CHADEMA, has declared a day of nation-wide demonstrations against what it calls the dictatorial tendencies of the Chama cha Mapinduzi (CCM) Government. The CCM Government has threatened to deal harshly with the demonstrators, who, on their part, have pledged to go ahead with the demonstrations.
    The CCM Government is fabricating a crisis where none need exist. It is not fate that is unfolding, but sheer hubris on the part of the powers that be. If the CCM Government has any sense, all it has to do is respect the Tanzanian constitution and the political parties act, which together recognize the people's right to peacefully assemble and hold demonstrations. CHADEMA has stated, repeatedly, that they are organizing peaceful demonstrations.
    In view of this declaration, repeated and amplified time and again, it is patently absurd and unconscionable for the CCM Government to resort to threats and intimidation, and to prepare for confronting with violence citizens who seek to exercise their fundamental rights. The CCM Government can go ahead with its evil schemes, but, eventually, justice will prevail, as it has always done everywhere, since time immemorial.

    ReplyDelete