KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

August 17, 2016

WAKUU WA WILAYA WALIOACHWA NA RAIS DK. MAGUFULI WAUNDA SACCOS

Mwenyekiti wa Umoja wa waliokuwa wakuu wa
 wilaya walioachwa na JPM, Ramadhani Maneno
 akizungumza wakati wa semina ya PSPF, jana
NA K-VIS BLOG/Khalfan Said
WAKUU wa wilaya wastaafu, walioteuliwa wakati wa Serikali ya awamu ya nne, wameunda Ushirika wa Kuweka na Kukopa (SACCOS), ikiwa ni moja ya maazimio waliyotoka yao baada ya semina ya mafunzo ya siku mbili, iliyolenga kuwaelimisha namna bora ya kuwa wajasiriamali.

Akitangaza azimio hilo, mwishoni mwa mafunzo hayo yaliyofadhiliwa na Mfuko wa Pensheni wa PSPF, na kufanyika makao makuu ya Mfuko huo jijini Dar es Salaam, Mjumbe wa Sekretariati ya wakuu hao wastaafu, Crispin Meela, alisema, wajumbe 10 wamechaguliwa na wana semina hao ili kushughulikia utaratibu mzima wa kuanzishwa kwa SACCOS hiyo haraka iwezekanavyo.

Wajumbe wa Kamati ya muda ya kusimamia mambo hayo ni pamoja na Ramadhan Maneno (Mwenyekiti), Betty Mkwasa (Katibu), Crispin Meela, Erasto Sima, Geogina Bundala, Farida Mgomi, Said Amanzi, Fatma Ally, Muhingo Rweyemamu na Manzie Mangochie.

Kwenye mafunzo hayo Wakuu hao wa wilaya wastaafu, waliweza kupata elimu kutoka kwa wataalamu mbalimbali wakiwemo Katibu Mtendaji wa Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi, Beng’ Issa, na wataalamu wa Saikolojia, na Wajasiriamali wenyewe kama vile Eric Shigongo.

Akifunga mafunzo hayo Mkurugenzi Mkuu wa PSPF, Adam Mayingu, ametoa changamoto kwa wakuu hao wanaokadiriwa kufikia 100 na ambao wamejiunga uanachama wa Mfuko huo kupitia mpango wa uchangiaji wa Hiari, (PSS), kuwa uamuzi wao utawakwamua kiuchumi na wanachotakiwa ni kuwa na mpango kamambe utakaoweza kutekelezeka kwa ufanisi mkubwa.

“PSPF kama shirika lingine lolote lile la kutoa huduma za Pensehni na za kifedha, umoja huo ni fursa kubwa kwa Mfuko na ndio maana umeamua kuwaunga mkono  ili mmfikie azma yenu ya kuanzisha SACCOS hiyo”. Alisema.
HABARI KATIKA PICHA

Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya Global Publishers, Eric Shigongo, akitoa mada juu ya ujasiriamali kwa Wakuu wa Wilaya wastaafu, wakati wa semina ya mafunzo ya ujasiriamali yaliyofadhiliwa na Mfuko wa Pensheni wa PSPF, na kufanyika makao makuu ya Mfuko huo jijini Dar es Salaam, Agosti 16, 2016.


 Mwenyekiti wa Wakuu wa wilaya wastaafu, Ramadhan Maneno
 Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, (TAMISEMI), George Simbachawene, (watatu waliokaa), Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Ashantu Kijaji, (wapili waliokaa), Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya PSPF, George Yambesi, (wapili kulia), Mkurugenzi Mkuu wa PSPF, Adam Mayingu, (wakwanza kushoto waliokaa) na Mwenyekiti wa Wakuu hao wa Wilaya wastaafu, Ramadhan Maneno, (wakwanza kulia waliokaa) wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wastaafu hao

No comments:

Post a Comment