KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

October 15, 2016

ASASI YAWAKUTANISHA VIJANA

Meneja Mradi, Ushirikishwaji wa Vijana - TYVA, Alfred Kiwuyo  akiwaelezea washiriki dhima ya kongamano la vijana waliokutana kujadili haki na wajabu kwa vijana katika maendeleo ya Taifa. (Picha na Geofrey Adroph)

TYVA  ni asasi ya vijana ambayo imejikita na Kujipambanua kupigania jamii yenye haki na usawa, amani na misingi ya kidemokrasia na yenye ushiriki hai na wenye tija kwa vijana katika shughuli za maendeleo imeandaa kongamano hili kuwawezesha vijana kujadili Haki na Wajibu kwa Vijana na mstakabali wa Taifa kwa ujumla. Kongamano hili pia lilikuwa na dhima ya kupanua uelewa na umuhimu wa vijana kushiriki kikamilifu katika shughuli za maendele ya Taifa kwa ujumla.
Wakili Chikulupi Kasaka, akitoa mada ya Haki na Wajibu wa Vijana kwa vijana mbalimbali wa vyoni na mtaani waliokuta kujadili haki na wajibu wao katika jamii iliyofanyika katika ukumbi wa British Council jijini Dar es salaam iliyoandaliwa na Taasisi la Vijana la TYVA .

Mwenyekiti wa Bodi ya washauri ya Vijana(YAB) Femina Hip, Hassan Pukey akitoa mada kwa vijana waliofika katika kongamano lililoandaliwa na Taasisi la Vijana la TYVA ili kujadili haki na wajibu wa vijana na katika jamii.

Makamu Mwenyekiti wa TYVA, Kamala Dickson akizungumzia mchakato wa baraza la vijana na jinsi vijana walivyoshirikishwa katika kutoa maoni ya mchakato mzima iliyoandaliwa na Taasisi la Vijana la TYVA na kufanyika katika ukumbi wa British Council jijini Dar es Salaam leo

No comments:

Post a Comment