KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

October 2, 2016

MCHENGELWA: KULA SAHANI MOJA NA WANAOINGIZA MIFUGO MIPYA RUFIJI

Na Mwamvua Mwinyi, Rufiji
al1MBUNGE  wa jimbo la Rufiji, mkoani Pwani, Mohammed Mchengelwa ameahidi kula sahani moja na baadhi ya viongozi wakiwemo wa vijiji ambao wanadaiwa kushirikiana na wafugaji kuingiza mifugo kiholela jimboni hapo.
Mbali na hilo amesema amejipanga kuvalia njuga suala la migogoro ya ardhi inayotokana na jamii ya wafugaji na wakulima.
Ameeleza pande hizo zimekuwa zikisigana mara kwa mara wakigombania maeneo hali inayosababisha kutokea kwa vurugu ambapo wakati mwingine hupelekea uvunjifu wa amani.
Aidha Mchengelwa alisema kuwepo kwa migogoro ya ardhi kwa wakulima na wafugaji  katika halmashauri ya Rufiji kunatokana na  baadhi ya wafugaji kuamua kuvunja sheria na taratibu zilizopo.

No comments:

Post a Comment