![]() |
Kwa
kutambua umuhimu wa michezo kwa vijana nchini, benki ya NMB imedhamini
vijana watano kutoka nchini kwa ajili ya kwenda kushiriki mashindano ya
mashua ya Afrika yanayotaraji kufanyika Luanda, Angola kuanzia Septemba,
6-13, mwaka huu.
Akizungumzia
udhamini huo wa Milioni 10 na jezi kwa vijana hao, Mkurugenzi Mtendaji
wa NMB nchini, Ineke Bussemaker amesema NMB kama benki ya kitanzania
inawathamini watanzania wote na inajivunia kuwa sehemu ya makampuni
ambao yameidhamini timu hiyo ili ikaiwakilishe nchi katika mashindano ya
mashua.
|
October 3, 2016
NMB YADHAMINI TIMU YA MASHUA MASHINDANO YA AFRIKA MASHARIKI
Subscribe to:
Post Comments (Atom)



No comments:
Post a Comment