![]() |
Miezi
sita baada ya aliyekuwa mtangazaji wa Clouds FM, Paul James (PJ) (Wa pili kushoto) na
mwenzake Gerard Hando kuondoka Clouds Fm na kuamia E Fm, mmoja wa
watangazaji hao, PJ amerejea Clouds Fm.
PJ
ametangazwa kurejea Clouds Fm na mtangazaji wa kipindi cha XXL, B Dozen
akianza kwa kukumbushia jinsi PJ alivyokuwa akisoma magazeti katika
kipindi cha Power Breakfast na baada ya hapo kumkaribisha kuzungumza.
Baada
ya kumtambulisha PJ alitumia fursa hiyo kuelezea jinsi safari yake ya
maisha ya kazi baada ya kuondoka Clouds Fm ilivyokuwa na kuwashauri
wenzake kuwa inabidi kufanya kazi kwa bidii ili kuleta mabadiliko
nchini.
“Hii
ni nchi yetu lazima tuijenge pamoja, lazima utambue thamani yako,
umesaidia nchi kitu gani, tujitahidi kufanya kitu chenye faida, inabidi
kutumia heshima na hekima kufanya kazi yako,
“Tuna
rais mzuri ana ndoto nyingi kwa ajili ya kuisaidia nchi sasa tufanye
kazi kumsaidia kazi rais wetu kazi ili afanikiwe kufanya kile
alichopanga kukifanya,” alisema PJ.
Aidha
PJ hajataja kwa sasa atakuwa anatangaza kipindi gani kati ya kipindi
alichokuwepo awali cha Power Breakfast au kipindi cha Jahazi baada ya B
Dozen kumuuliza ili wasikilizaji wajue watamsikia muda gani akitangaza.
|
October 5, 2016
PAUL JAMES SWEYA (PJ)AREJEA CLOUDS FM
Subscribe to:
Post Comments (Atom)



No comments:
Post a Comment