Mkuu wa
Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda (katikati), akizungumza na
wanafunzi wa kidato cha nne wa Shule ya Sekondari ya Jitegemee JKT
Mgulani katika mahafali ya 32 yaliyofanyika jana. Makonda alikuwa mgeni
rasmi. Kulia ni Mkuu wa Shule hiyo, Luteni Kanali Robert Kessy na
kushoto ni Mwenyekiti wa Bodi wa Shule hiyo, Brigedia Generali Laurance
Magere.
RC Makonda akimkabidhi cheti Mwalimu Bora wa Shule hiyo, Grace Eliyatosha Moshi.
RC Makonda akimkabidhi zawadi Mwanafunzi Bora, Samuel Ndebeto.
RC
Makonda akipeana mkono na mhitimu wa kidato cha nne wa Shule ya
Sekondari ya Jitegemee JKT, Samina Rajab baada ya kumkabidhi cheti
katika mahafali ya 32 kwa ushiriki wake wa masuala ya Skauti shuleni
hapo. Katikati ni Mwenyekiti wa Bodi wa Shule hiyo, Brigedia Generali Laurance Magere.
Huyu ndiye ni Mwanafunzi Bora wa Shule hiyo, Samuel Ndebeto.


No comments:
Post a Comment