Mwanamuziki
wa kike kutoka nchini Marekani, Toni Braxton amefikishwa hospitalini
kwa kusumbuliwa na ugonjwa wa mfumo wa kinga wa mwili (Lupus), baada ya
kuzidiwa wakati akiwa katika maandalizi ya kufanya onyesho mjini
Cleveland, Marekani.
Katika
taarifa iliyotolewa kupitia ukurasa wake wa Twitter, ilieeleza kuwa
msanii huyo hali yake ya kiafya ilibadilika ghafla hivyo ikabidi
afikishwe hospitali na kwa watu wote ambao tayari walikuwa wameshanunua
tiketi wazitunze kwani watatangaziwa tarehe nyingine ya onyesho.
“Toni
Braxton yupo hospitali mjini Cleveland baada ya kulalamika kusumbuliwa
na lupus. Kwa bahati mbaya onyesho lake la usiku Cleveland
limesimamishwa,” ilisema taarifa hiyo na kuongeza.
“Lupus
inahitaji kufuatiliwa kwa umakini kwa muda na hili haliwezi kusababisha
kusimamishwa kwa ziara yote, tiketi kwa ajili ya onyesho la leo
zitunzwe na ratiba ya tarehe nyingine itatajwa haraka iwezekanavyo”
Toni
alifahamika kuwa na ugonjwa wa Lupus mwaka 2011 na kwa mwezi Oktoba
pekee ameshafikishwa hospitalini mara mbili baada ya hali ya kiafya kuwa
mbaya hivyo kutakiwa kupatiwa huduma ya haraka.


No comments:
Post a Comment